-
Russia na Hizbullah zataka kufunguliwa ofisi ya uwakilishi Moscow
Apr 07, 2021 03:12Serikali ya Russia na Harakati ya Hizbullah ya Lebanon zinatafakari kuhusu uwezekano wa kufunguliwa ofisi ya uwakilishi ya harakati hiyo ya muqawama katika mji mkuu wa Russia, Moscow.
-
Naim Qassim: Kushikamana Waislamu kumesambaratisha njama za US-Israel
Apr 01, 2021 06:05Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuungana na kushikamana Waislamu pasina kujali tofauti zao za kimitazamo na kiitikadi kumesambaratisha njama za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel za kuyagawanya vipande vipande mataifa ya Kiislamu.
-
Lebanon yalaani madai ya utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu Hizbullah
Mar 17, 2021 23:18Balozi wa Lebanon katika Umoja wa Mataifa amelaani madai yaliyotolewa hivi karibuni na viongozi wa Kizayuni dhidi ya Hizbullah akisisitiza kuwa hayana msingi na yanaingilia masuala ya ndani ya nchi yake.
-
Israel yakiri; Hizbullah inaweza kuvurumisha makombora 2,000 kwa siku dhidi yake
Mar 17, 2021 01:06Kamanda wa ngazi ya juu wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel amekiri kuwa, harakati ya Hizbullah ya Lebanon ina uwezo wa kuvurumisha makombora elfu mbili kwa siku dhidi ya utawala huo haramu iwapo makabiliano ya kijeshi yataibuka baina ya pande hizo katika siku za usoni.
-
Hizbullah yasema itaendelea kusimama na Iran mkabala wa Marekani
Feb 21, 2021 04:12Naibu Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema harakati hiyo ya muqawama itaendelea kusimama bega kwa bega na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kukabiliana na Marekani.
-
Hizbullah yalaani mauaji ya mkosoaji wa harakati hiyo ya Lebanon
Feb 05, 2021 08:44Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imelaani vikali mauaji ya mwanaharakati wa kisiasa na mtafiti wa nchi hiyo ya Kiarabu, Lokman Slim aliyeuawa katika mazingira ya kutatanisha.
-
Israel inayahofu makombora yenye shabaha kali ya Hizbullah ya Lebanon
Jan 16, 2021 10:11Mchambuzi wa masuala ya kijeshi wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel amesema, utawala huo umeingiwa na hofu na kiwewe kwa sababu ya makombora yenye shabaha kali ya harakati ya muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Nasrallah: Lengo la kuuawa kigaidi Soleimani na Abu Mahdi Al Muhandis lilikuwa ni kuhuisha ISIS
Sep 30, 2020 03:33Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema magaidi wa Marekani walilenga kuhusisha kundi la kigaidi la ISIS walipowaua shahidi Luteni Jenerali Haj Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) na Abu Mahdi al Muhandis, Naibu Kamanda wa Kikosi cha Kujitolea cha Wananchi wa Iraq (Hashd al Shaabi).
-
Ufaransa yakadhibisha madai ya Marekani dhidi ya Hizbullah
Sep 19, 2020 08:19Wizara ya Mambo ya Nje ya Ufaransa imesema hakuna ushadidi wowote unaoonyesha kuwa tawi la kijeshi la harakati ya Hizbullah ya Lebanon limefanya magendo ya kemikali kwa ajili ya kutengeneza mada za mlipuko nchini Ufaransa, kama inavyodai Marekani.
-
Nasrullah: Mapambano ya Hizbullah hayaishii ndani ya mipaka ya Lebanon
Aug 23, 2020 03:20Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kutekeleza majukumu kwa ajili ya kuisaidia jamii yote ya wanadamu ni jambo la wajibu kwa mujibu wa thamani za Uislamu, na kwamba mipaka ya kijografia na kisiasa haipaswi kuwa kizingiti cha kutekeleza wajibu huo.