-
Al Manar: Kamanda wa jeshi la utawala wa Kizayuni aangamizwa kwenye oparesheni ya Hizbullah ya Lebanon
Sep 01, 2019 12:46Televisheni ya al Manar imetangaza kuwa harakati ya Hizbullah ya Lebanon imeangamiza moja ya zana za kijeshi za Israel katika barabara ya al Thakna katika mji wa mpakani wa Israel wa Avivim na kumuua kamanda wa kikosi kimoja wa jeshi la utawala wa Kizayuni huko kaskazini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu katika oparesheni iliyotekelezwa na harakati ya Hizbullah.
-
Sheikh Naeem Qasim: Muqawama ndio nguzo ya mapambano dhidi ya utawala wa Kizayuni
Aug 04, 2019 20:56Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa harakati hiyo pamoja na taifa na jeshi la Lebanon ni nguzo muhimu ya mapambano dhidi ya hujuma za utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hizbullah: Utawala wa Kizayuni wa Israel hauheshimu haki za kimsingi za watoto
Aug 01, 2019 03:27Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel hauheshimu haki za kimsingi kabisa za watoto na unapuuza makubaliano ya kimataifa yanayohusiana na haki hizo.
-
Hizbullah: Lebanon hatuna hofu na vitisho vya utawala haramu wa Israel
Jul 26, 2019 08:07Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah nchini Lebanon amesema kuwa, kwa kutegemea uwezo wake wa ndani, Lebanon haina hofu yoyote na vitisho vya utawala haramu wa Kizayuni.
-
Jumanne tarehe 16 Julai 2019
Jul 15, 2019 22:18Leo ni Jumanne tarehe 13 Dhulqaada 1440 Hijria sawa na Julai 16 mwaka 2019.
-
"Siasa za Marekani dhidi ya Iran zimefeli"
Jul 07, 2019 22:12Naibu wa Mkuu wa Baraza la Utendaji la Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, siasa za serikali ya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimefeli.
-
Hizbullah: Utatuzi wa kadhia ya Palestina kwa fedha ni udhalilishaji mkubwa
Jun 24, 2019 23:06Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Harakati ya Muqawama ya nchini Lebanon Hizbulla, amesema kuwa, mtazamo wa Marekani kwa wananchi wa Palestia kuwa ni watu masikini ambao matatizo yao yanatatuliwa tu kwa fedha, ni udhalilishaji mkubwa kwa watu wa taifa hilo.
-
Hizbullah: Hatua ya Iran kutungua ndege ya ujasusi ya Marekani, ni sisitizo la kujilinda
Jun 22, 2019 22:03Kaimu Mkuu wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah nchini Lebanon sambamba na kuashiria hatua ya kutunguliwa na Iran ndege ya ujasusi isiyo na rubani ya Marekani, amesema kuwa hatua hiyo inathibitisha kwamba Tehran haitofumbia macho kukiukwa kwa haki yake ya kujitawala.
-
Hizbullah: Utawala haramu wa Israel ndio chimbuko kuu la ugaidi duniani
Apr 19, 2019 23:54Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah nchini lebanon, Sheikh Naim Qassem amesema kuwa, utawala haramu wa Kizayuni wa Israel ndio chanzo kikuu cha ugaidi na uharibifu katika eneo la Asia Magharibi na duniani kwa ujumla.
-
Nasrullah: Hatua ya US dhidi ya IRGC ni thibitisho kuwa Washington imefeli katika eneo
Apr 11, 2019 09:26Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon (Hizbullah) sambamba na kulaani hatua ya Rais Donald Trump ya kuliweka Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC katika orodha ya Marekani ya makundi ya kigaidi amesisitiza kuwa, kitendo hicho ni ithibati tosha kuwa Washington imefeli katika njama zake ghalati katika eneo la Asia Magharibi.