-
Jihad Islami: Kuanzisha uhusiano na adui Mzayuni ni khiyana na usaliti kwa Palestina
Dec 13, 2021 05:59Harakati ya Jihad Islami ya Palestina imelaani vikali kitendo cha viongozi wa Imarati cha kumpokea nchini humo Naftali Bennett, Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel na kueleza kwamba, hiyo ni khiyana na usaliti kwa taifa la Palestina.
-
Raisi: Iran inaunga mkono usalama wa nchi za pambizoni mwa Ghuba ya Uajemi
Dec 06, 2021 23:23Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa usalama wa nchi za eneo la Ghuba ya Uajemi unafungamana na kwamba Iran inaunga mkono usalama wa nchi za pambizoni mwa Ghuba ya Uajemi.
-
Shamkhani: Usalama na uthabiti wa Asia Magharibi utapatikana kwa kuweko ushirikiano wa kikanda
Dec 06, 2021 09:35Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa kuweko ushirikiano wa mataifa ya Asia Magharibi ni jambo la dharura na la lazima kwa ajili ya kupatikana amani na usalama wa eneo hili.
-
Licha ya kujitweza, Saudia na UAE zinamdhalilisha Mansour Hadi
Dec 03, 2021 00:56Licha ya rais wa zamani wa Yemen aliyejiuzulu na kutoroka nchi, Abdu Rabbuh Mansour Hadi kujipendekeza na kujitweza kwa Saudi Arabia na Imarati, lakini watawala wa Riyadh na Abu Dhabi wameendelea kumdhalilisha na kumtolea vitisho mwanasiasa huyo wa Yemen mwenye umri wa miaka 76.
-
"Jenerali mtesaji" wa Imarati ateuliwa kuongoza Polisi ya Kimataifa (Interpol)
Nov 25, 2021 11:02Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) limemteua Jenerali wa Imarati aneyetuhumiwa kutesa watu kuwa mkuu wake mpya kufuatia mkutano wake wa kila mwaka uliofanyika mjini Instanbul Uturuki.
-
Safari ya mrithi wa ufalme wa Imarati nchini Uturuki; sababu na malengo yake
Nov 25, 2021 04:07Mohammed Bin Zayed Al Nayhan, mrithi wa ufalme wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) jana Jumatano tarehe 24 Novemba aliwasili mjini Ankara, Uturuki ambapo alikutana na kufanya mazungumzo na Rais Recep Tayyip Erdoğan wa nchi hiyo.
-
Baada ya miaka 10, Waziri wa Mambo ya Nje wa Imarati aitembelea Syria
Nov 09, 2021 23:09Vyombo vya habari vya Kiarabu vimetangaza kuwa baada ya kupita kipindi cha miaka 10, Waziri wa Mambo ya Nje wa Imarati (UAE) amefanya safari ya kuitembelea Syria.
-
Shirika la ujasusi la Kizayuni lafungua ofisi yake ya uwakilishi Abu Dhabi, UAE
Oct 01, 2021 09:59Duru za habari zimeripoti kuwa, shirika moja la kizayuni linalotengeneza vifaa vya intaneti vya ujasusi limefungua ofisi yake mjini Abu Dhabi, katika Umoja wa Falme za Kiarabu.
-
Gazeti lafichua waraka wa siri wa njama ya Imarati ya kuibana na kuidhoofisha HAMAS
Sep 29, 2021 09:31Gazeti la al Akhbar linalochapishwa nchini Lebanon limefichua waraka wa siri unaohusu mpango wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) wa kuanzisha muungano dhidi ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS.
-
Nukta kadhaa za kuzingatia kuhusu madai ya Imarati ya kupambana na ugaidi
Sep 15, 2021 05:48Umoja wa Falme za Kiarabu, Imarati, umeongeza majina ya watu 38 na mashirika 15 katika orodha yake ya watu wanaodaiwa kuunga mkono ugaidi ambapo majina ya Wairani kadhaa yanaonekana katika orodha hiyo.