-
Majaji Wakuu wa Jumuiya ya Shanghai wamuenzi Shahidi Raisi
May 23, 2024 06:55Majaji Wakuu na Wenyeviti wa Mahakama za Juu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) wamenyamaza kimya kwa dakika moja kumuenzi Shahidi Ebrahim Raisi, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maafisa wenzake walioaga dunia katika ajali ya helikopta iliyotokea Jumapili iliyopita katika mkoa wa Azarbaijan Mashariki, kaskazini magharibi mwa Iran.
-
Viongozi wa nchi 68 watoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Sayyid Raisi na ya wenzake
May 22, 2024 11:26Viongozi na maafisa wakuu wa nchi 68 duniani leo wamefika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Tehran kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Rais Sayyid Ebrahim Raisi na ya wenzake waliokufa shahidi pamoja naye katika ajali ya helikopta iliyotokea siku ya Jumapili.
-
Kiongozi wa Mapinduzi amhutubu Haniya: Ahadi ya Allah ya kutokomezwa utawala wa Kizayuni itatimia
May 22, 2024 09:16Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza katika mazungumzo na Ismail Haniya, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Hamas na ujumbe alioandamana nao kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kutokomezwa utawala wa Kizayuni itatimia.
-
Bendera ya Umoja wa Mataifa yapepea nusu mlingoti kuwaenzi mashahidi wa ajali ya helikopta ya Iran
May 21, 2024 23:19Umoja wa Mataifa umepeperusha bendera yake nusu mlingoti ikiwa ni ishara ya heshima kwa wahanga wa ajali ya helikopta nchini Iran iliyowahusisha Rais Ebrahim Raisi, Waziri wa Mambo ya Nje Hossein Amirabdollahian na maafisa wengine wakuu.
-
Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran asisitiza kusitishwa mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel
May 21, 2024 09:02Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ametilia mkazo kusitishwa mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni na kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina.
-
Katibu Mkuu wa UN atuma rambirambi kufuatia kufa shahidi Ebrahim Raisi na wenzake
May 21, 2024 08:56Antonio Guterres Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametuma salamu za rambirambi kwa familia za shahidi Rais Sayyid Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wenzake aliokuwa amefuatana nao na kutoa mkono wa pole kwa serikali na wananchi wa Iran.
-
Kaimu Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aarifishwa rasmi Umoja wa Mataifa
May 21, 2024 08:51Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa wa Mataifa katika barua rasmi kwa Umoja wa Mataifa amewaarifisha katika taasisi hiyo ya kimataifa Kaimu Rais na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kuwa viongozi wa muda katika nyadhifa hizo.
-
Iran yatangaza tarehe ya uchaguzi wa rais; Sayyid Raisi kuzikwa Alkhamisi
May 21, 2024 03:50Iran imetangaza Juni 28, 2024 kuwa tarehe ya kufanyika uchaguzi wa rais, kufuatia kufa shahidi Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu katika ajali ya helikopta iliyotokoea Jumapili katika mkoa wa Azarbaijan Mashariki, kaskazini magharibi mwa Iran.
-
Serikali: Uchaguzi wa rais wa Iran utafanyika ndani ya siku 50
May 20, 2024 04:19Msemaji wa Baraza la Kulinda Katiba ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema baraza maalumu litaundwa kwa ajili ya kuandaa mazingira ya kufanyika uchaguzi wa rais katika kipindi cha siku 50 zijazo.
-
Viongozi wa dunia wasikitishwa na kifo cha Rais wa Iran
May 20, 2024 03:54Viongozi wa mataifa mbali mbali duniani wameendelea kutoa mkono wa pole kufuatia vifo vya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Ebrahim Raisi pamoja na wenzake kadhaa katika ajali ya helikopta iliyotokea jana katika mkoa wa Azarbaijan Mashariki, kaskazini magharibi mwa Iran.