-
Kana'ani: Mkakati wa Iraq kuzipatanisha Iran, Saudia mzizi wake ni Soleimani
Mar 16, 2023 07:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameashiria mapatano ya kurejesha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia na kueleza kuwa, msingi wa jitihada za Iraq za kuzipatanisha Tehran na Riyadh unatokana na mitazamo ya kistratajia ya Shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC).
-
Katibu Mkuu wa Arab League: Kupatana Tehran na Riyadh ni hatua chanya kwa maana halisi
Mar 15, 2023 04:08Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amesema makubaliano yaliyofikiwa kati ya Iran na Saudi Arabia ni hatua nzuri na chanya kwa maana yake halisi na akaongeza kuwa athari zake za kwanza ni kupatikana kwa namna fulani utulivu wa kisiasa na kiusalama kati ya nchi hizo mbili.
-
Tehran, mwenyeji wa kongamano la kubainisha ubaguzi na jinai za Israel
Mar 14, 2023 22:54Kongamano la kupambana na ubaguzi na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina lilifanyika jana Jumanne hapa Tehran, mji mkuu wa Iran na kuhudhuria na wajumbe wa makundi ya muqawama ya Palestina, maafisa wa Jamhuri ya Kiislamu na wa nchi kadhaa za Kiarabu.
-
Libya: Mapatano kati ya Iran na Saudi Arabia ni kwa maslahi ya nchi za Asia Magharibi
Mar 12, 2023 23:12Wizara ya Mambo ya Nje ya Libya imetoa taarifa na kukaribisha mapatano yaliyofikiwa kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia na kueleza kuwa, mapatano hayo yana maslahi kwa nchi mbili na eneo zima la Asia Magharibi kwa ujumla.
-
Iran yakosoa undumakuwili wa Ufaransa juu ya suala la haki za binadamu
Mar 12, 2023 04:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani undumakuwili wa Ufaransa, ambayo kwa upande mmoja inajinadi kuwa mbeba bendera ya kutetea haki za binadamu, lakini kwa upande wa mwngine inakanyaga haki hizo kwa vitendo.
-
Ofisi ya UN: Mapatano ya Iran, Saudia yataharakisha usitishaji vita Yemen
Mar 12, 2023 04:08Ofisi ya ubalozi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa imepongeza mapatano ya kurejesha tena uhusiano wa kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Kiislamu na Saudi Arabia na kueleza kuwa, muafaka huo utaharakisha mchakato wa kusitishwa vita na mapigano nchini Yemen.
-
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu yapongeza mapatano baina ya Iran na Saudia
Mar 11, 2023 23:27Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imepongeza mapatano ya kurejesha tena uhusiano wa kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia na kueleza kuwa, hiyo ni hatua muhimu katika uga wa kuimarisha amani na uthabiti katika eneo la Asia Magharibi.
-
Makundi ya mapambano ya Palestina yakaribisha mapatano baina ya Iran na Saudia
Mar 11, 2023 07:07Makundi mbalimbali ya Wapalestina yamekaribisha makubaliano ya kurejesha tena uhusiano kati ya Tehran na Riyadh kwa kutoa taarifa tofauti.
-
Abdollahian: Umefika wakati vikosi vamizi viondoke Syria mara moja
Mar 10, 2023 04:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema vikosi vya nchi ajinabi vinapaswa kuondoka katika ardhi ya Syria haraka iwezekanavyo.
-
US yaziwekea vikwazo taasisi 39 kwa kuisaidia Iran 'kukwepa' vikwazo vya kifedha
Mar 10, 2023 04:06Marekani imetangaza kuyawekea vikwazo makumi ya mashirika kwa tuhuma za kuisaidia Iran kukwepa vizingiti vya Washington vya kuiweka Tehran nje ya mfumo wa kimataifa wa fedha.