-
Mufti wa Oman: Mapatano ya Iran na Saudia yameutia hofu na kiwewe utawala wa Kizayuni wa Israel
Mar 18, 2023 00:37Mufti wa Oman Sheikh Ahmad bin Hamad Al-Khalili amesisitiza haja ya kudumishwa amani na utangamano katika eneo la Ghuba ya Uajemi na kubainisha kwamba, makubaliano na mapatano yaliyofikiwa kati ya Iran na Saudi Arabia yameutia hofu na kiwewe utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Mazoezi ya pamoja ya majeshi ya majini ya Iran, China na Russia
Mar 16, 2023 22:45Mazoezi ya pamoja ya majeshi ya majini ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, China na Russia yanayofanyika kwa anwani ya "Ukanda wa Amani wa Baharini 2023", yameakisiwa sana kimataifa na kuwa habari ya kwanza katika vyombo mashuhuri vya habari duniani.
-
Msimamo wa Iran kwa mnasaba wa Machi 15, Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Chuki dhidi ya Uislamu
Mar 16, 2023 08:17Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran jana Jumatano alituma ujumbe katika ukurasa wake wa Twitter akisema kwamba: Wale wenye chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu hawaamini maadili yoyote ya kibinadamu na dini za Mwenyezi Mungu.
-
Iran, China na Russia zafanya luteka ya pamoja katika Bahari ya Oman
Mar 16, 2023 07:55Vikosi vya majini vya Iran, Russia na China vinaendelea na mazoezi ya pamoja ya kijeshi katika Bahari ya Oman, huo ukiwa ni muendelezo wa juhudi za nchi tatu hizo za kuimarisha ushirikiano wa majeshi yao ya baharini.
-
Kana'ani: Mkakati wa Iraq kuzipatanisha Iran, Saudia mzizi wake ni Soleimani
Mar 16, 2023 07:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameashiria mapatano ya kurejesha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia na kueleza kuwa, msingi wa jitihada za Iraq za kuzipatanisha Tehran na Riyadh unatokana na mitazamo ya kistratajia ya Shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC).
-
Katibu Mkuu wa Arab League: Kupatana Tehran na Riyadh ni hatua chanya kwa maana halisi
Mar 15, 2023 04:08Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amesema makubaliano yaliyofikiwa kati ya Iran na Saudi Arabia ni hatua nzuri na chanya kwa maana yake halisi na akaongeza kuwa athari zake za kwanza ni kupatikana kwa namna fulani utulivu wa kisiasa na kiusalama kati ya nchi hizo mbili.
-
Tehran, mwenyeji wa kongamano la kubainisha ubaguzi na jinai za Israel
Mar 14, 2023 22:54Kongamano la kupambana na ubaguzi na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina lilifanyika jana Jumanne hapa Tehran, mji mkuu wa Iran na kuhudhuria na wajumbe wa makundi ya muqawama ya Palestina, maafisa wa Jamhuri ya Kiislamu na wa nchi kadhaa za Kiarabu.
-
Libya: Mapatano kati ya Iran na Saudi Arabia ni kwa maslahi ya nchi za Asia Magharibi
Mar 12, 2023 23:12Wizara ya Mambo ya Nje ya Libya imetoa taarifa na kukaribisha mapatano yaliyofikiwa kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia na kueleza kuwa, mapatano hayo yana maslahi kwa nchi mbili na eneo zima la Asia Magharibi kwa ujumla.
-
Iran yakosoa undumakuwili wa Ufaransa juu ya suala la haki za binadamu
Mar 12, 2023 04:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani undumakuwili wa Ufaransa, ambayo kwa upande mmoja inajinadi kuwa mbeba bendera ya kutetea haki za binadamu, lakini kwa upande wa mwngine inakanyaga haki hizo kwa vitendo.
-
Ofisi ya UN: Mapatano ya Iran, Saudia yataharakisha usitishaji vita Yemen
Mar 12, 2023 04:08Ofisi ya ubalozi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa imepongeza mapatano ya kurejesha tena uhusiano wa kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Kiislamu na Saudi Arabia na kueleza kuwa, muafaka huo utaharakisha mchakato wa kusitishwa vita na mapigano nchini Yemen.