-
Safari ya Waziri wa Ulinzi wa China mjini Tehran; ukurasa mpya katika uhusiano wa kiulinzi na kijeshi wa pande mbili
Apr 28, 2022 02:41Jenerali Wei Fenghe, Waziri wa Ulinzi wa China aliwasili mjini Tehran siku ya Jumatano kwa ajili ya kuonana na kufanya mazungumzo na Brigedia Jenerali Mohammad Reza Gharaei Ashtiani, Waziri mwenzake wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rais wa Iran aipongeza Afrika Kusini kwa kuadhimisha Siku ya Taifa
Apr 27, 2022 22:20Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtumia ujumbe wa pongezi mwenzake wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa kwa mnasaba wa taifa hilo la Kiafrika kuadhimisha Siku ya Taifa.
-
Raisi: Maafisa wa ngazi za juu wa Iran na China wana nia ya kupanua uhusiano wa kimkakati.
Apr 27, 2022 08:46Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika mazungumzo yake na Waziri wa Ulinzi wa China kuwa: Viongozi wa ngazi za juu wa Tehran na Beijing wana nia ya dhati ya kupanua uhusiano wa kistratijia wa muda mrefu bila ya kujali matukio ya kimataifa.
-
Sisitizo la Iran la kurudishwa amani ya kudumu katika eneo kwa kuondolewa ukaliwaji mabavu wa ardhi za Palestina
Apr 22, 2022 03:46Hussein Amir Abdollahian, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa amani ya kudumu katika eneo la Asia Magharibi itapatikana tu kwa kuondolewa kikamilifu ukaliwaji mabavu wa ardhi za Palestina, kurejea wakimbizi wote katika ardhi zao za jadi na kuainishwa mfumo wa utawala wa baadaye wa Palestina kwa msingi wa kura ya maoni pamoja na kuundwa serikali huru katika ardhi hizo.
-
Al-Jazeera: Iran imeionya Israel, yaiambia maghala yako ya silaha yatalengwa
Apr 22, 2022 02:41Televisheni ya Al-Jazeera ya Qatari imeripoti kuwa, Iran imetuma picha na ramani za maghala ya silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni kwa serikali ya Tel Aviv kupitia nchi moja ya Ulaya.
-
Iran yalaani kuvunjiwa heshima matukufu ya Kiislamu na vitendo vya mabavu dhidi ya Waislamu nchini Uswidi
Apr 19, 2022 06:25Ali Bahadori Jahromi, Msemaji wa Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameandika katika ukurasa wake binafsi wa kijamii akijibu vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu barani Ulaya hususan nchini Uswidi kwamba: “Uhuru wa kidini umebadilishwa kuwa kukashifiwa dini za mbinguni, na uhuru wa kujieleza umekuwa chombo cha kueneza misimamo mikali na ubaguzi wa rangi katika nchi za Magharibi."
-
Kenya na Iran kuimarisha uhusiano wao katika nyuga za utalii na uwekezaji
Apr 19, 2022 03:38Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kenya zimeazimia kusaini makubaliano ya maelewano juu ya kuimarisha uhusiano wa pande mbili katika nyuga za uwezekaji na utalii.
-
Drone "Gaza" ya Jeshi la Sepah la Iran yafaulu majaribio na kuanza kufanya kazi kikamilifu
Apr 18, 2022 22:30Ndege mpya isiyo na rubani ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) iliyopewa jina la Gaza, imefaulu majaribio ya kuruka na sasa inafanya kazi kikamilifu.
-
Raisi aionya Israel isithubutu kuichokoza Iran hata kidogo
Apr 18, 2022 03:40Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uwezo wa majeshi ya Iran ni uwezo wa kumzuia adui na kuongeza kuwa, uchokozi hata mdogo zaidi wa maadui kama vile utawala wa Kizayuni wa Israel hautafumbiwa macho na vikosi vya ulinzi vya Iran.
-
Iran yawaasa Waislamu duniani waungane kuwatetea Wapalestina, Msikiti wa Aqsa
Apr 16, 2022 22:56Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran kwa mara nyingine tena amelaani jinai ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuushambulia na kuuvunjia heshima Msikiti wa al-Aqsa na kusisitiza kuwa, mataifa ya Kiislamu yanapaswa kuungana na kusima bega kwa bega kuitetea kadhia ya Palestina.