-
Iran: Marekani haina chaguo jingine isipokuwa kukubali uhalisia wa mambo
Nov 23, 2021 04:03Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ambaye anaongoza timu ya mazungumzo ya Jamhuri ya Kiislamu na kundi la 4+1 yatakayoanza Novemba 29 huko Vienna amesema kuwa, Marekani sharti ikubali hali halisi ya mambo kwa kufungamana na ahadi ilizotoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Iran yataja sababu ya kuenea uhalifu na ugaidi kote duniani
Nov 23, 2021 00:00Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema sababu kuu ya kuenea uhalifu na ugaidi katika maeneo mbalimbali ya dunia ni magendo na biashara haramu ya silaha nyepesi na ndogo.
-
Iran yasikitishwa na hali mbaya ya wakimbizi wa Afghanistan
Nov 22, 2021 08:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameeleza wasi wasi wake kuhusu hali mbaya inayowakabili wakimbizi wa Afghanistan.
-
Jeshi la Majini la Iran limetoa vipigo 6 ndani ya miezi 18 dhidi ya Marekani
Nov 21, 2021 08:04Kamanda wa Kikosi cha Majini cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema jeshi hilo la Iran limetoa pigo mara sita dhidi ya Wamarekani katika Ghuba ya Uajemi katika kipindi cha miezi 18 iliyopita.
-
Haniya: Iran ni nguzo muhimu ya kambi ya muqawama
Nov 21, 2021 08:01Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) ameipongeza Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kuitaja kama nguzo kuu na muhimu ya mrengo wa muqawama wa Wapalestina.
-
Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran kwa kisingizio cha kuingilia uchaguzi
Nov 20, 2021 10:13Wizara ya Fedha ya Marekani juzi Alhamisi ilitangaza kuwa imeyaweka katika orodha yake ya vikwazo majina ya shakhsia sita na shirika moja la Iran kwa kisingizio cha kuingilia uchaguzi wa rais wa Marekani. Ofisi inayosimamia fedha ya taasisi hiyo ya Marekani imesema kuwa imeyaweka katika orodha yake ya vikwazo majina ya watu sita na taasisi moja ya Iran kwa kile ilichokitaja kuwa kujaribu kuathiri uchaguzi wa rais wa Marekani wa mwaka 2020.
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Sahihi ya rais wa Marekani si ya kutegemewa
Nov 19, 2021 11:50Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema, sharti la kukubaliwa Marekani kurudi kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni kuondoa Washington kwa namna athirifu, itakayoweza kuthibitika na kwa wakati mmoja vikwazo vyote ilivyoiwekea Iran na kwamba sahihi ya rais wa Marekani haiwezi kutegemewa.
-
"Vikwazo vipya dhidi ya Iran ni muendelezo wa sera zilizofeli za Trump"
Nov 19, 2021 04:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu si kitu kingine ghairi ya muendelezo wa sera zilizogonga ukuta za Donald Trump.
-
Lengo la Tehran kushiriki vikao vya Vienna ni kutaka kuondolewa Iran vikwazo vyote haramu
Nov 18, 2021 23:36Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema lengo kuu la Tehran kushiriki mazungumzo ya Vienna kuhusu mapatano ya nyuklia ya JCPOA yanayotazamiwa kuanza mwishoni mwa mwezi huu ni kuhakikisha kuwa taifa la Iran linaondolewa vikwazo vyote haramu.
-
Iran: IAEA iache pupa inapozungumzia masuala ya nyuklia
Nov 17, 2021 23:27Kaimu Mwakilishi wa Iran katika taasisi za kimataifa zenye makao yao huko Vienna, Austria ameziasa nchi wanachama wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) zijiepushe kutoa taarifa kwa haraka bila mazingatio juu ya makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.