-
Iran, Russia zasisitiza mazungumzo ya JCPOA yatafanikiwa Iran ikiondolewa vikwazo
Oct 29, 2021 23:57Iran na Russia zimesisitiza kwamba mazungumzo ya pande zilizosalia katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA ya mwaka 2015 yatafanikiwa tu iwapo yatapelekea kuondolewa vikwazo dhidi ya Iran sambamba na pande zote kutekeleza mapatano hayo.
-
Uhusiano wa kiuchumi wa Iran na Saudi Arabia waanza rasmi, meli ya kwanza ya Iran yatia nanga Saudia
Oct 28, 2021 03:55Mkuu wa Shirikisho la Usafirishaji Nje Bidhaa za Iran amesema kuwa, uhusiano wa kiuchumi wa nchi yake na Saudi Arabia umeanza rasmi baada ya meli moja yenye bidhaa za Iran kutia nanga katika moja ya bandari za Saudia.
-
Rais Ebrahim Raisi alaani hujuma ya kimtandao dhidi ya vituo vya mafuta vya Iran
Oct 27, 2021 23:08Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, shambulio la kimtandao dhidi ya vituo vya mafuta vya Jamhuri ya Kiislamu ni njama za maadui zilizolenga kuwahamakisha na kuvuruga maisha ya kila siku ya Wairani.
-
Njia pekee ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Afghanistan ni kuzishirikisha kaumu zote katika muundo wa kisiasa
Oct 27, 2021 23:02Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi Jrani na Afghanistan mwishoni mwa kikao chao hapa Tehran wametoa taarifa ya pamoja na kusisitiza kuwa: njia pekee ya kuupatia ufumbuzi mgogoro wa Afghanistan ni kuasisi muundo mpana wa kisiasa kwa kuyashirikisha makundi yote ya nchi hiyo.
-
Iran na EU zajadili namna ya kuondolewa vikwazo vyote haramu katika JCPOA
Oct 27, 2021 10:28Ofisi ya uwakilishi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Ulaya imetangaza kuwa, kuondolewa vikwazo vyote haramu na visivyo vya kisheria ilivyoekewa Iran ndio ajenda kuu ya mazungumzo ya Brussels kati ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa na mratibu wa kamisheni ya pamoja ya makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Mkutano wa pili wa Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa mataifa jirani na Afghanistan+Russia waanza Tehran
Oct 27, 2021 04:42Mkutano wa pili wa Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa mataifa jirani na Afghanistan+Russia umeanza kufanyika hapa mjini Tehran kwa shabaha ya kujadili changamoto mbambali zinazoikabili nchi hiyo baada ya majeshi ya Marekani kuondoka nchini humo na wanamgambo wa Taliban kuchukua hatamu za uongozi wa nchi.
-
Rais wa Iran ayataka madola ya Ulaya kuwa na mamlaka katika kuchukua maamuzi
Oct 25, 2021 07:26Rais Ibrahim Raeisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kusisitiza kuwa, madola ya Ulaya yanapaswa kuwa na mamlaka katika kuchukua maamuzi amesema kuwa, maataifa hayo hayapaswi kufanya mambo kwa namna ambayo yataifanya Marekani kuyaona kama sehemu yake ya kupenya na kupitishia mambo yake.
-
Ulimwengu wa Michezo, Oktoba 25
Oct 25, 2021 05:26Hujambo mpenzi msikilizaji na hususan mfuatiliaji wa masuala ya spoti natumai hujambo hapo ulipo. Karibu tutupie jicho baadhi ya matukio muhimu ya michezo yaliyojiri ndani ya siku saba zilizopita katika pembe mbalimbali za dunia....
-
Iran iko tayari kushirikiana na nchi za Kiislamu katika uga wa nyuklia
Oct 24, 2021 11:43Msemaji wa Taasisi ya Nishati ya Atomiki ya Iran (AEOI) amesema Jamhuri ya Kiislamu ipo tayari kushirikiana na nchi za Kiislamu katika sekta ya nishati ya nyuklia.
-
Rais wa Iran atuma salaamu maalumu za Maulidi na kuzaliwa Mtume (saw) kwa viongozi wa nchi za Kiislamu
Oct 23, 2021 23:55Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Ebrahim Raisi ametuma salamu maalumu na mkono wa baraka na fanaka kwa viongozi wa nchi za Kiislamu kwa mnasaba wa maadhimisho ya Maulidi na siku ya kuzaliwa Mtume wa Mwisho wa Mwenyezi Mungu, Muhammad (saw) na Wiki ya Umoja wa Kiislamu.