-
Hati ya ushirikiano mpana wa kistratijia wa Iran na China na wasiwasi wa Wamagharibi
Apr 16, 2021 22:11Tarehe 29 Machi mwaka huu, Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na China walitia saini hati ya ushirikiano mpana wa kistratijia wa nchi mbili, kufuatia safari ya Wang Yi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Watu wa China mjini Tehran, ikiwa ni katika kukaribia maadhimisho ya kutimia miaka 50 ya uhusiano wa kidiplomasia wa Tehran na Beijing.
-
Araqchi: Nchi za Ulaya zinapaswa kuonyesha zinayapa uzito mazungumzo ya nyuklia
Apr 16, 2021 03:22Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Tume ya Pamoja ya Mapatano ya Nyuklia ya JCPOA ilifanya kikao chake Vienna, Austria jana Alhamisi ambapo kikao hicho kilikuwa na changamoto nyingi.
-
Admeri Khanzadi: Adui hana ubavu wa kuhujumu maji ya Iran
Apr 15, 2021 23:04Kamanda wa Jeshi Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema maadui hawana ubavu wala uthubutu wa kuhujumu maji ya taifa hili.
-
Wazayuni wana wasiwasi wa Iran kulipiza kisasi cha hujuma dhidi ya kituo cha nyuklia cha Natanz
Apr 15, 2021 09:08Waziri mkuu wa zamani wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel amesema, ana wasiwasi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuchukua hatua ya kulipiza kisasi kwa sababu ya Israel kufanya hujuma katika kituo cha nyukulia cha Natanz.
-
Kimya cha IAEA baada ya uharibifu uliofanywa katika taasisi ya nyuklia ya Iran
Apr 14, 2021 21:55Hujuma ya uharibifu iliyofanywa na Israel katika taasisi ya nishati ya nyuklia ya Natanz nchini Iran siku ya Jumapili iliyopita, kwa mara nyingine tena imeleta udharura wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kama taasisi kuu zaidi ya kimataifa inayosimamia shughuli za nyuklia dunia, kutoa jibu na kueleza wazi msimamo wake.
-
Kiongozi Muadhamu: Sera za Iran kuhusu JCPOA ziko wazi
Apr 14, 2021 12:41Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amezungumza kuhusu mapatano ya nyuklia ya JCPOA na vikwazo na kusema sera za Iran ziko wazi kuhusu JCPOA na vikwazo. Ameongeza kuwa sera hizo amezibainisha wazi kwa wakuu wa nchi kupitia maandishi na katika mikutano.
-
Vikwazo vipya vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Iran; kwenda sambamba na Washington na Tel Aviv
Apr 14, 2021 08:18Baraza la Umoja wa Ulaya Jumatatu tarehe 12 mwezi huu wa Aprili liliwajumuisha maafisa 8 na taasisi 3 katika ordha ya vikwazo dhidi ya Iran kwa kisingizio cha eti kukiuka haki za binadamu. Aidha baraza hilo limechukua uamuzi wa kurefusha hatua zake dhidi ya Iran hadi tarehe 13 mwezi Aprili mwaka kesho kwa kisingizio cha kile ilichokitaja kuwa ukiukaji wa haki za binzdamu.
-
Chanjo ya Corona ya Barekat kuanza kuzalishwa kwa wingi nchini Iran wiki ijayo
Apr 13, 2021 03:24Mwenyekiti wa Ofisi Kuu ya Kutekeleza Maagizo ya Imam Khomeini amesema Wakfu wa Barekat wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran utaanza kuzalisha kwa wingi chanjo ya kukabiliana na virusi vya Corona ya 'COVIran Barekat' kuanzia wiki ijayo Aprili 21.
-
Iran yawapongeza Waislamu kwa kuwadia mwezi wa Ramadhani
Apr 13, 2021 02:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewapongeza na kuwatakia Waislamu wote duniani kheri na baraka kwa mnasaba wa kuwadia mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Iran yasitisha mazungomzo kamili na Umoja wa Ulaya
Apr 12, 2021 23:10Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikwazo ambavyo Umoja wa Ulaya (EU) umeweka dhidi ya baadhi ya taasisi na maafisa wa Iran. Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Saeed Khatibzadeh amesema kufuatia vikwazo hivyo, Iran inasitisha kwa muda mazungumzo yake kamili na Umoja wa Ulaya yakiwemo yale yanahohusu haki za binadamu.