-
Viongozi wa Marekani waendeleza misimamo yao ya kiuadui dhidi ya Iran
Dec 15, 2020 04:38Ikiwa ni katika kudumisha misimamo ya uhasama ya viongozi wa White House dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, mjumbe maalumu wa serikali ya Marekani anayeshughulikia masuala ya Iran ameunga mkono vikwazo vya Washington dhidi ya Tehran.
-
Zanganeh: Iran haihitaji idhini ya kurejea katika soko la mafuta
Dec 14, 2020 08:57Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Bijan Namdar Zangeneh amesema taifa hili halihitaji idhini yoyote kurejea katika soko la mafuta na kwamba lina uwezo wa kuuza mapipa milioni 2.3 ya mafuta kila siku.
-
Iran yalalamikia taarifa ya Ufaransa ya kumuunga mkono mhalifu aliyenyongwa
Dec 14, 2020 01:20Iran imemuita balozi wa Ufaransa mjini Tehran Philippe Thiebaud kulalamikia taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya nchi hiyo ya Ulaya ambayo imelaani kutekelezwa hukumu ya kunyongwa Ruhullah Zam, aliyepatikana na hatia ya kusimamia mtandao uliokuwa ukiendesha propaganda chafu dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Jumapili, 13 Disemba, 2020
Dec 12, 2020 22:19Leo ni Jumapili tarehe 27 Mfunguo Saba Rabiu Thani mwaka 1442 Hijria sawa na tarehe 13 Disemba 2020 Miladia.
-
Iran: Marekani inawashawishi wengine watoe muhanga kadhia ya Palestina
Dec 12, 2020 03:51Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema Marekani inazishawishi nchi zingine kutoa muhanga kadhia ya Palestina na kuwapa mkono wezi kwa njia mbali mbali.
-
Kinara wa propaganda za ghasia anyongwa Iran
Dec 12, 2020 03:37Ruhullah Zam, kinara wa mtandao wa habari wa Amad News ambao ulikuwa unaeneza propagadna dhidi ya Mapinduzi ya Kiislamu amenyongwa kufuatia hukumu iliyotoelwa na mahakama.
-
Watu 232 wengine wafariki dunia kwa corona nchini Iran
Dec 11, 2020 09:54Msemaji wa Wizara ya Afya, Tiba na Mafunzo ya Utabibu ya Iran amesema kuwa, watu wengine zaidi ya elfu 9 wameambukizwa kirusi cha corona na wengine 232 wamefariki dunia katika kipindi cha masaa 24 yaliyopita.
-
Madai ya uongo ya Marekani kuhusu kuondolewa dawa na vifaa vya matibabu katika vikwazo vya nchi hiyo dhidi ya Iran
Dec 10, 2020 13:00Baada ya Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia mashuhuri kama JCPOA mwano Mei 2018, nchi hiyo imeiwekea Iran vikwazo vikali zaidi chini ya siasa za 'mashinikizo ya juu kabisa', na tokea wakati huo imekuwa ikiongeza vikwazo hivyo visivyo vya kibinadamu bila kujali kuenea nchini na duniani virusi vya maradhi hatari ya corona.
-
Feisal Miqdad: Uhusiano wa Iran na Syria ni mkubwa na wa kistratejia
Dec 09, 2020 03:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amesema kuwa uhusiano wa Tehran na Damascus ni mkubwa na wa kistratejia na kueleza kuwa: Syria ina uhusiano mkubwa na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja zote za kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni.
-
Katibu Mkuu wa Arab League atoa bwabwaja nyingine dhidi ya Iran na Uturuki
Dec 08, 2020 03:52Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) amepayuka tena dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki, katika hotuba yake mbele ya wanachuo mjini Cairo Misri.