-
Bahreini: Uvamizi wa Israel dhidi ya Qatar, tishio kwa usalama wa eneo na kimataifa
Sep 16, 2025 23:13Balozi wa Iran katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva, Uswisi amelaani vikali uvamizi wa karibuni wa utawala wa Israel dhidi ya Qatar na kuitolea wito jamii ya kimataifa kuchukua hatua kuzuia kuendelea vitendo kama hivyo ambavyo vinatishia kila mtu katika kanda hii.
-
Rais Pezeshkian: Saudi Arabia inabeba 'jukumu zito' kwa umoja wa Waislamu dhidi ya Israel
Sep 16, 2025 08:42Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa mataifa makubwa ya Kiislamu, hasa Saudi Arabia yanabeba "jukumu zito sana" katika hali ya sasa, na kwamba kuwepo umoja kati ya nchi za Kiislamu kutazuia uchokozi wa Israel.
-
Baqaei: Rasimu ya azimio inasisitiza kuzuiwa mashambulizi dhidi ya taasisi za nyuklia za malengo ya kiraia
Sep 16, 2025 08:41Esmail Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran ametoa taarifa kuhusu rasimu ya azimio la Iran katika Mkutano Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) unaoendelea Vienna, Austria ambayo inalenga kuzuia mashambulizi kwenye vituo vya nyuklia vinavyoendesha shughuli zake kwa malengo ya amani na ya kiraia.
-
Rais wa Iran azitahadharisha nchi za Kiislamu Doha: Hakuna nchi itakayokuwa salama na uchokozi wa Israel
Sep 16, 2025 04:12Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema mashambulizi ya Israel ya Septemba 9 dhidi ya Qatar yameonyesha kuwa hakuna nchi ya Kiarabu au ya Kiislamu iliyo salama kutokana na vitendo vya uchokozi vya utawala huo.
-
Jumanne, 16 Septemba 2025
Sep 16, 2025 03:42Leo ni Jumanne tarehe 23 Mfunguo Sita Rabiul Awwal 1447 Hijria sawa na Septemba 16, 2025.
-
Iran yatwaa taji la ubingwa wa dunia wa Miereka 2025, yaziacha nyuma Russia na Marekani
Sep 16, 2025 03:18Timu ya taifa ya mchezo wa miereka aina ya Freestyle ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Mashindano ya Dunia ya Miereka ya mwaka 2025 yanayofanyika mjini Zagreb, Croatia kwa kunyakua jumla ya medali tano na kulitwaa taji hilo kabla ya muda wa mashindano kumalizika.
-
Araghchi: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko bega kwa bega na Qatar na Waislamu wote
Sep 15, 2025 02:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ambaye yuko mjini Doha, Qatar kushiriki katika mkutano wa dharura wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi za Kiislamu na Kiarabu, amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu iko bega kwa bega na ndugu zake Waislamu wote.
-
Juhudi za mhimili wa Magharibi za kuchafua jina la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Sep 14, 2025 04:46Wanachama wa Mchakato wa Radiamali ya Haraka wa Kundi la G7 ambazo ni nchi za Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan, Uingereza, Marekani na Umoja wa Ulaya, pamoja na Australia na New Zealand, katika taarifa ya pamoja siku ya Ijumaa walidai kulaani hatua za Iran kuhusiana na eti kuongezeka kwa kampeni ya ukandamizaji unaotekelezwa nje ya mipaka yake.
-
Larijani azitaka serikali za Kiislamu kuchukua hatua dhidi ya jinai za Israel
Sep 13, 2025 08:02Ali Larijani, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran katika ujumbe wake amezitaka serikali za Kiislamu kuchukua hatua madhubuti na za kivitendo dhidi ya jinai za Israel.
-
Araghchi aikosoa Ulaya kwa kufumbia macho uchokozi wa US, Israel dhidi ya Iran
Sep 12, 2025 03:41Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi ameyajia juu mataifa matatu ya Ulaya kwa mtazamo wao wa "kutowajibika" mkabala wa uchokozi wa hivi karibuni wa Marekani na Israel dhidi ya Iran, pamoja na vitisho vyao vya kuhuisha maazimio yaliyobatilishwa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, jambo ambalo anaamini litazidisha tu mivutano iliyopo.