-
Makabiliano ya kidiplomasia yajiri kati ya Iran, Marekani na Saudia katika Umoja wa Mataifa
Oct 13, 2018 04:40Mjumbe wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Kamati ya Kwanza ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa amewakabili wawakilishi wa Marekani na Saudi Arabia katika umoja huo na kuwaeleza kwamba, utawala wa kifalme wa Saudia ni utawala wa kigaidi ambao hata waandishi wa habari pia hawasalimiki na mauaji ya kigaidi yanayofanywa na utawala huo.
-
Ndoto za Trump za kuuondoa madarakani utawala wa Kiislamu nchini Iran
Oct 12, 2018 23:13Kamanda wa Jeshi la Wazlini wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (Sepah) amesema kuwa: Rais Donald Trump wa Marekani anakosea kwa kudhani kuwa Iran imedhoofika baada ya yeye kushika madaraka ya nchi huko Marekani.
-
Trump awashambulia marafiki na maadui zake
Oct 11, 2018 23:11Tangu aingie madarakani nchini Marekani mwezi Januari 2017, Rais Donald Trump wa nchi hiyo amekuwa akitekeleza siasa ambazo zimeifanya dunia kuwa uwanja wa malumbano na mivutano.
-
Njama za kikundi cha Munafiqeen na uchochezi dhidi ya Iran
Oct 11, 2018 08:13Kukamatwa mwanadiplomasia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Ubelgiji kwa tuhuma bandia za kushiriki kwake katika mpango wa kushambuliwa kikundi cha kigaidi cha Munafigeen katika mojawapo ya viunga vya Paris, mji mkuu wa Ufaransa, ni uchochezi mpya dhidi ya Iran.
-
Iran: Suala la kutia dosari ushirikiano wa Syria na shirika la OPCW linapasa kuepukwa
Oct 10, 2018 11:27Balozi na Mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Shirika Linalopiga Marufuku Silaha za Kemikali (OPCW) amezungumzia kuangamizwa silaha za kemikali huko Syria na kusisitiza kuwa suala la kuchafua ushirikiano mkubwa unaotolewa na Damascus kwa shirika hilo linapasa kuepukwa.
-
Ndege za Qatar Airways kuendelea na safari za Iran licha ya vikwazo vya Marekani
Oct 09, 2018 04:33Shirika la ndege la Qatar Airways limesema safari za ndege za shirika hilo za kwenda na kutoka Iran zitaendelea kama kawaida, licha ya vikwazo vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Iran yaitaka jamii ya kimataifa ishirikiane kupambana na sera za kibeberu za US
Oct 09, 2018 04:27Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amezitaka nchi za dunia kuimarisha ushirikiano wao ili zifanikiwe kuzikabili sera za kibeberu na za kibabe za Marekani.
-
Afrika Kusini yapongeza ushindi wa Iran dhidi ya Marekani katika mahakama ya ICJ
Oct 07, 2018 04:18Idara ya Uhusiano na Ushirikiano wa Kimataifa ya Afrika Kusini imepongeza hatua ya Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ) kuiagiza Washington isimamishe vikwazo vyake vya upande mmoja dhidi ya Iran haraka iwezekanavyo.
-
Ufaransa: Marekani haina haki ya kuchukua maamuzi kwa niaba ya Ulaya
Oct 06, 2018 03:46Waziri wa Fedha wa Ufaransa amesema kuwa, Marekani haiwezi kuchukua maamuzi kuhusiana na ushirikiano wa kibiashara wa nchi za Ulaya na Iran na kuongeza kuwa, vikwazo vya serikali ya Washington dhidi ya Iran ni fursa kwa Ulaya kwa ajili ya kuanzisha taasisi zinazojitegemea za kifedha.
-
"Makombora, jibu na ujumbe wa Iran kwa waungaji mkono wa ugaidi"
Oct 05, 2018 12:15Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran sanjari na kupongeza mashambulizi ya makombora yaliyofanywa na Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC dhidi ya ngome za magaidi nchini Syria amesema operesheni hiyo ilikuwa jibu la Iran lililobeba ujumbe mahsusi kwa magaidi, wafadhili na waungaji mkono wao.