-
Marekani yakiri kuwa haiwezi kuingia kwenye vita vya kijeshi na Iran
Dec 17, 2017 04:26Waziri wa Ulinzi wa Marekani amekiri kuwa Washington haina mpango wowote wa kuanzisha vita vya kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kutokana na tuhuma kuwa Tehran inaizatiti kwa silaha harakati ya Ansarullah ya Yemen.
-
Zarif: Iran itaishtaki Marekani Umoja wa Mataifa
Dec 17, 2017 00:16Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kwamba Jamhuri ya Kiislamu itayawasilisha Umoja wa Mataifa madai ya Nikki Haley, balozi wa Marekani katika umoja huo kwamba eti Iran imeipatia silaha harakati ya Ansarullah ya Yemen.
-
Zarif: Uhai na kifo cha baadhi ya nchi zinazopakana Iran unategemea amri ya madola makubwa
Dec 16, 2017 12:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Mohammad Javad Zarif amesema uhai na kifo cha baadhi ya tawala zinazopakana na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran unategemea maamuzi ya madola makubwa au Shirika la Kijeshi ya Nchi za Magharibi (NATO), au madola makubwa ya nyuklia.
-
Uganda yaalika mashirika zaidi ya Iran kuwekeza nchini humo
Dec 16, 2017 12:00Spika wa Bunge la Uganda ametoa wito kwa mashirika ya Iran yaimarishe zaidi uwekezaji nchini humo.
-
Kambi ya muqawama yenye mshikamano; mwokozi dhidi ya njama za maadui
Dec 16, 2017 04:34Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, SEPAH amesema kuwa, muqawama wa Kiislamu Mashariki ya Kati na dunia unaishia katika kambi ya muqawama wa Mapinduzi ya Kiislamu na kwamba ushindi mtawalia wa kambi hii ungali unaendelea.
-
Zarif: Marekani ni mshirika wa Saudia katika uhalifu wa kivita Yemen
Dec 16, 2017 00:15Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa Marekani ni mshirika wa Saudi Arabia katika uhalifu na jinai za kivita zinazofanyika nchini Yemen.
-
Maonyesho bandia ya Marekani dhidi ya Iran hayatafanikiwa
Dec 15, 2017 03:27Gholamali Khoshroo mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amepinga vikali tuhuma za Balozi wa Marekani katika umoja huo dhidi ya Iran kuhusu msaada wa silaha kwa vikosi vya Yemen. Amesema tuhuma hizo ni ishara ya wazi ya uharibifu, uchochezi na kutowajibika Marekani.
-
UN: Kombora lililovurumishwa Riyadh Saudi Arabia si la Iran
Dec 15, 2017 00:47Naibu msemaji wa Umoja wa Mataifa usiku wa kuamkia leo amesisitiza kuwa, hakuna ushahidi wowote unaoweza kuthibitisha madai kwamba makombora yanayotumiwa na jeshi la Yemen kuipiga Saudi Arabia yanatoka nchini Iran.
-
Katibu Mkuu wa UN: Makombora yaliyoshambulia Saudia kutokea Yemen si ya Iran
Dec 12, 2017 12:53Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema umoja huo haujaweza kuthibitisha kuwa makombora yaliyolenga uwanja wa ndege wa Mfalme Khalid katika mji mkuu wa Saudi Arabia, Riyadh ni ya Iran.
-
Jenerali Qassem Soleimani: Iran iko tayari kuvisaidia vikosi vya Muqawama vya Palestina kwa kila hali
Dec 12, 2017 12:48Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) ametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kutoa msukumo na kuvisaidia kwa kila hali vikosi vya Muqawama wa Kiislamu wa Palestina.