-
Umuhimu wa Mkutano wa Kimataifa wa Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran
May 18, 2025 10:54Mkutano wa Kimataifa wa Jukwaa la Mazungumzo ya Tehran unafanyika kwa kuwashirikisha takriban wageni 200 kutoka nchi 53 duniani. Mkutano huo umefunguliwa rasmi mapema leo katika hafla iliyohudhuriwa na Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Waziri wa Mambo ya Nje, Abbas Araqchi.
-
Pezeshkian: Iran inafanya mazungumzo, lakini haigopi vitisho vyovyote
May 17, 2025 10:30Rais Masoud Pezeshkian amesisitiza kuwa, Iran haitasalimu amri na kuachana na haki zake licha ya vitisho, akieleza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitaachana na mafanikio yake ya heshima katika nyanja yoyote ile, iwe kisayansi au kijeshi.
-
Iran: Israel iliundwa kwa damu; mauaji ya kimbari lazima yakomeshwe sasa
May 16, 2025 07:22Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kwa mnasaba wa Siku ya Nakba na kusema kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel "uliasisiwa katika msingi wa umwagaji damu" na kwamba jamii ya kimataifa ina wajibu wa kukomesha mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza.
-
Trump azitaka kampuni za US zitengeneze droni kama za Iran
May 16, 2025 07:01Rais wa Marekani, Donald Trump amesema ameziomba kampuni za Marekani kutengeneza ndege zisizo na rubani zinazofanana na droni za Iran, ambazo si ghali sana bali zina kasi ya juu na hatari.
-
Ansarullah: Iran imetekeleza wajibu wake wa Kiislamu kuiunga mkono Palestina
May 16, 2025 06:52Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen ameipongeza Iran kwa uungaji mkono wake usio na kikomo kwa taifa la Palestina na kadhia yao halali na kueleza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu inafuata njia ya heshima katika suala hilo na nchi nyingine zote za Kiislamu lazima zifuate mkondo huo.
-
Iran kuishtaki "Google" kwa kupotosha jina la "Ghuba ya Uajemi"
May 15, 2025 04:05Kituo cha Kitaifa cha Anga za Juu cha Iran kimesema kitachukua hatua za kisheria dhidi ya kampuni ya Google ya Marekani na majukwaa mengine ya kimataifa kutokana na kupotoshwa kwa jina la kihistoria la Ghuba ya Uajemi.
-
Araghchi: Matamshi ya Trump juu ya Iran huko Riyadh ni ya "udanganyifu"
May 15, 2025 03:10Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amepuuzilia mbali matamshi ya Rais wa Marekani, Donald Trump kuhusu ustawi na maendeleo ya Iran kuwa ya "udanganyifu" akiashiria vikwazo vya Washington dhidi ya nchi hii kwa zaidi ya miongo minne.
-
Iran: Hakuna haja ya kuendelea na mazungumzo iwapo Marekani....
May 14, 2025 11:30Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi amesisitiza kuwa haki ya Jamhuri ya Kiislamu ya kurutubisha madini ya urani ni "mstari mwekundu" wa taifa hili, akisisitiza kuwa, kufikiwa makubaliano na Marekani kuhusu mpango wa amani wa nyuklia wa nchi hii kunategemea kufuata kanuni hizo.
-
Baqaei: Kusimamisha miradi ya nyuklia ya Iran kimsingi si jambo linalojadiliwa katika mazungumzo na Marekani
May 14, 2025 06:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa suala la kusimamisha miradi ya nyuklia ya Iran kimsingi halijadiliwi katika mazungumzo na Marekani na kwamba miradi yetu ya nyuklia bila shaka itaendelea kwa jadi.
-
Iran yailaani Israel kwa kupiga mabomu kambi za wakimbizi Palestina
May 14, 2025 02:47Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali mashambulizi ya hivi karibuni ya anga dhidi ya kambi za wakimbizi wa Kipalestina yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel na kusababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa makumi ya Wapalestina wasio na hatia wakiwemo watoto wadogo.