-
Pezeshkian: Iran imeazimia kuimarisha uhusiano na Algeria
Nov 01, 2024 23:30Rais wa Iran Masoud Pezeshkian ameipongeza Algeria kwa kuadhimisha miaka 70 ya mapinduzi yake, akielezea utayarifu wa Iran wa kuimarisha uhusiano na nchi hiyo ya Kiarabu katika nyuga mbali mbali.
-
Qaani: Kikosi cha Quds cha IRGC kitakuwa pamoja na Hizbullah hadi kuangamizwa Uzayuni
Nov 01, 2024 03:41Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran amempongeza Sheikh Naim Qassim kwa kuchaguliwa kuwa Katibu Mkuu mpya wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon na kusema: Kikosi cha Quds kitakuwa pamoja na Hizbullah hadi utakapotokomezwa mti habithi wa Uzayuni na kukombolewa Palestina na Quds Tukufu.
-
Lavrov: Mkataba wa ushirikiano wa ulinzi kati ya Russia na Iran utatiwa saini hivi karibuni
Nov 01, 2024 03:39Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia ametangaza kuwa makubaliano ya ushirikiano wa pamoja wa ulinzi kati ya Moscow na Tehran yatatiwa saini hivi karibuni.
-
Rais Pezeshkian: Umoja utawafanya Waislamu kuwa na nguvu kubwa
Oct 31, 2024 22:57Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya umoja baina ya nchi za Kiislamu na kusema: Iwapo tutaweza kufikia umoja katika nyanja za kiuchumi, kisiasa na kijamii, tunaweza kuwa nguvu kubwa katika eneo la Asia Magharibi, na katika hali hii Marekani haiwezi kutuwekea vikwazo.
-
Iran yaendelea na jitihada za kusimamishwa vita Ghaza na Lebanon
Oct 31, 2024 03:41Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo na mawaziri wenzake wa mambo ya nje wa Misri, Indonesia na Qatar na kujadiliana nao masuala ya kikanda na uhusiano wa pande mbili ikiwa ni muondelezo wa jitihada za Iran za kuhakikisha vita vinakomeshwa huko Ghaza na Lebanon.
-
Iran: Tutajibu iwapo Israel itarusha hata mshale jangwani
Oct 30, 2024 23:07Vyombo vya ulinzi vya Iran vimesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo ya uchokozi wowote wa Israel dhidi ya ardhi yake, hata kama hatua hiyo ni ndogo na isiyo na tija, kama kurusha mshale kuelekea kwenye jangwa moja la nchi hii.
-
Iran: Tunao uwezo wa kuishambulia Israel kwa 'darzeni' za operesheni sawa na "Ahadi ya Kweli"
Oct 30, 2024 10:04Waziri wa Ulinzi Brigedia Jenerali Aziz Nasirzadeh amesema Iran inao uwezo wa kuteketeza 'darzeni' za operesheni za kulipiza kisasi sawa na "Operesheni ya Ahadi ya Kweli" iliyotekeleza mwezi Aprili kulenga maeneo ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi ya Palestina unayoikalia kwa mabavu.
-
Malalamiko ya wajumbe wa Baraza la Usalama dhidi ya ushirikiano wa Marekani na utawala wa Kizayuni
Oct 30, 2024 06:35Katika kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichofanyika karibuni kwa ajili ya kijadili suala la hujuma ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, nchi nyingi zikiwemo Algeria, China, Russia, Iraq na Syria zimelaani vikali kitendo hicho cha uchokozi na kutaka uchokozi huo ukomeshwe mara moja.
-
Iran: Tuna haki halali ya kujilinda na kujihami
Oct 30, 2024 00:00Msemaji wa serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani amesema Jamhuri ya Kiislamu ina haki ya kujilinda na kusisitiza kuwa, nchi hii itatekeleza haki hiyo "halali" kwa "wakati na mahali mwafaka."
-
Araghchi: Baraza la Usalama linapasa kuiwekea vikwazo Israel
Oct 30, 2024 00:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lina jukumu la kuuwekea vikwazo utawala wa Kizayuni wa Israel kutokana na tabia ya utawala huo kuendelea kushupalia vita na umwagaji damu huko Gaza na Lebanon.