Aug 24, 2024 11:08
Matokeo ya uchunguzi wa maoni uliofanywa na taasisi ya habari ya Mako ndani ya jamii ya Wazayuni yanaonyesha kuwa asilimia 75 ya Waisraeli hawaridhishwi na namna serikali ya waziri mkuu wa utawala huo Benjamin Netanyahu inavyoshughulikia hali ya usalama kwenye mpaka wa kaskazini, ambako kila siku kunaandamwa na mashambulio makali ya Harakati ya Muqawama wa Kiisilamu ya Hizbullah ya Lebanon tangu Israel ilipoanzisha vita dhidi ya Ukanda wa Ghaza Oktoba 7, 2023.