-
Kutimuliwa askari vamizi wa Marekani ndilo hitajio kuu la wananchi wa Iraq na Syria
Feb 10, 2019 23:19Mahdi Taqee, Mjumbe wa Kamisheni ya Usalama na Ulinzi ya Bunge la Iraq amesema kuwa, hadi sasa jumla ya wabunge 70 wa nchi hiyo wameshatia saini muswada wa kisheria wa kushinikiza kutimuliwa nchini humo askari wa kigeni hususan wa Marekani.
-
Ayatullah Sistani: Iraq haipasi kuwa kituo cha kuzidhuru nchi nyingine
Feb 06, 2019 11:50Kiongozi mkuu wa kidini nchini Iraq Ayatullah Ali Sistani amesisitiza kuwa Iraq haipasi kuwa kituo kinachotumiwa kwa ajili ya kuzidhuru nchi nyinginezo.
-
Iraq: Hatutaruhusu ardhi yetu itumike kuihujumu nchi yeyote ile
Feb 06, 2019 03:37Waziri Mkuu wa Iraq amekosoa matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump aliyedai kuwa wanajeshi wa Marekani wataendelea kuwepo nchini Iraq kwa shabaha ya kuipiga darubini Iran.
-
Maveterani wa UK: Tuliamrishwa tuwaue kwa kuwapiga risasi raia Iraq, Afghanistan
Feb 05, 2019 23:13Jeshi la Uingereza liliwaagiza askari wake wawaue kwa kuwafyatulia risasi raia wa Iraq na Afghanistan hata kama hawakuwa wamejizatiti kwa silaha.
-
Iraq yaionya Israel: Msifikirie kabisa kushambulia ardhi yetu
Jan 27, 2019 23:14Mjumbe wa Kamisheni ya Usalama na Ulinzi ya Bunge la Iraq ametoa onyo kali kwa utawala wa Kizayuni wa Israel na kuuonya usifikirie kabisa kushambulia ardhi ya nchi hiyo.
-
Jahangiri: Kama Iran isingelizisaidia Iraq na Syria, sasa hivi magaidi wangelikuwa na dola lao katika eneo hili
Jan 27, 2019 12:03Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kama Tehran isingelizisaidia Baghdad na Damascus katika mapambano yao dhidi ya magenge ya kigaidi, basi sasa hivi magenge hayo yangelikuwa yanazitawala nchi hizo.
-
Harakati ya Nujabaa Iraq: Kuwekewa vikwazo muqawama ni matokeo ya kufeli njama za Marekani
Jan 22, 2019 11:41Kiongozi wa Baraza la Kisiasa la Muqawama wa Kiislamu la Harakati ya Nujabaa nchini Iraq amesema kuwa, vikwazo vilivyowekwa na Marekani dhidi ya muqawama, vinaonyesha kufeli njama za Washington katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Al Hashdu sh-Sha'abi: Mashambulizi yetu dhidi ya Daesh huko Syria yameua na kujeruhi magaidi 35
Jan 19, 2019 04:08Kamanda wa Operesheni za mkoa wa Al Anbar za Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi nchini Iraq amesema kuwa, katika mashambulizi ya jana ya harakati hiyo dhidi ya ngome za magaidi wa kundi la Daesh (ISIS), magaidi 35 wa genge hilo wameuawa na kujeruhiwa.
-
Al Hashdu sh-Sha'abi yashambulia ngome za magaidi wa Daesh Deir ez-Zor, Syria
Jan 18, 2019 23:31Harakati ya Wananchi ya al Hashdu sh-Sha'abi nchini Iraq imefanya shambulizi dhidi ya ngome na maeneo ya magaidi wa kundi la Daesh (ISIS) katika mkoa wa Deir ez-Zor nchini Syria, ambapo kwa akali magaidi 15 wameangamizwa.
-
Kumalizika safari ya Zarif nchini Iraq; dhihirisho la urafiki kuanzia Baghad hadi Arbil
Jan 18, 2019 07:43Safari ya siku tano ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Baghdad na kukutana kwake na viongozi wa serikali kuu mjini Baghdad na wa eneo la Kurdistan nchini humo ni ishara inayodhihirisha wazi kwamba uhusiano wa nchi mbili hizi jirani ni wa kirafiki.