-
Polisi wa Iraq wagundua mahandaki mawili ya magaidi wa Daesh (ISIS)
Jun 20, 2018 11:49Polisi wa Federali ya Iraq imetangaza leo kuwa, imefanikiwa kugundua mahandaki mawili ya genge la kigaidi la Daesh (ISIS) katika eneo la Khuwaja na kutegua zaidi ya mabomu 10 yaliyokuwa yametegwa kwenye mahandaki hayo.
-
Waziri Mkuu wa Iraq: Waliochoma moto masanduku ya kura wamelenga moja kwa moja usalama na demokrasia yetu
Jun 11, 2018 09:36Waziri Mkuu wa Iraq amesema kuwa, moto uliotokea katika kituo kimoja kikuu cha kuhifadhia masanduku ya kura mjini Baghdad, ni njama zenye lengo la kutoa pigo kwa usalama na demokrasia ya nchi hiyo.
-
Kituo cha kuhifadhia masanduku ya kura za uchaguzi wa bunge la Iraq chateketea kwa moto
Jun 10, 2018 22:12Wizara ya Mambo ya Ndani ya Iraq imetangaza kuwa kituo cha kuhifadhia masanduku ya kura za uchaguzi wa bunge uliofanyika hivi karibuni nchini humo kimeteketezwa na moto.
-
Harakati ya Nujabaa: Daesh ni mradi wa Marekani kwa ajili ya kufikia malengo yake
Jun 10, 2018 12:18Katibu Mkuu wa Harakati ya Muqawama ya Nujaba ya nchini Iraq amesema kuwa, kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) ni njia nzuri ya Marekani kwa ajili ya kufikia malengo yake ya kikoloni na kiuchumi kupitia kisingizio cha kupambana na ugaidi katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Iraq yamtimua mwanadiplomasia wa Saudia
Jun 07, 2018 03:26Serikali ya Iraq imemtimua mwanadiplomasia mmoja wa Saudia kwa tuhuma za kuingilia uchaguzi wa bunge uliopita nchini humo.
-
Kufichuliwa njama ya Marekani ya kuingiza tena magaidi nchini Iraq
Jun 07, 2018 02:21Matukio ya mwaka mmoja uliopita nchini Iraq ambapo magaidi wakufurishaji wa ISIS au Daesh wamesambaratishwa na kutumiliwa kikamilifu kutoka maeneo yote waliyokuwa wameyateka kufuatia jitihada za jeshi na makundi ya kujitolea ya wananchi, yameiandaa Iraq kuingia duru mpya ya baada ya Daesh na kuandaa mazingira ya uchaguzi wa bunge uliofanyika mwezi uliopita.
-
Bunge la Iraq lataka zoezi la kuhesabu kura za uchaguzi lirudiwe tena
Jun 06, 2018 22:47Bunge la Iraq limeamua katika kikao cha dharura kilichofanyika hapo jana kuwa kura zote zilizopigwa katika uchaguzi wa bunge uliofanyika hivi karibuni zihesabiwe tena kwa mkono.
-
Muungano wa kijeshi wa Marekani wakiri kuua raia 892 wa Syria na Iraq
Jun 01, 2018 03:13Muungano wa kimataifa unaoongozwa na Marekani wa eti kupambana na kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) umekiri kupitia ripoti uliyotoa hapo jana kuwa tangu yalipoanza mashambulio ya anga ya muungano huo mwaka 2014 hadi sasa raia 892 wameuawa katika nchi za Syria na Iraq.
-
Seneta McCain akiri kuwa vita vya Iraq vilikuwa "kosa kubwa" ambalo lilifanywa na Marekani
May 27, 2018 02:44John McCain, seneta mwenye misimamo mikali amekiri japo kwa kuchelewa kuwa Marekani ilifanya makosa kuanzisha vita vya kuivamia kijeshi Iraq mwaka 2003.
-
Mazungumzo ya kuunda serikali mpya yanaendelea nchini Iraq
May 23, 2018 10:01Rais Fuad Masum wa Iraq na ujumbe wa Umoja wa Kitaifa wa Kurdisan leo wameitisha kikao cha kujadili uchaguzi wa hivi karibuni wa nchi hiyo na njia za kushirikiana makundi ya Kikurdi na mirengo mingine bungeni.