-
Kanisa la Kiprotestanti la Marekani: Israeli ni dola la ubaguzi wa rangi (apartheid)
Jul 10, 2022 03:43Mkutano Mkuu wa Kanisa la Kiprotestanti la Presbyterian la Marekani, huko Louisville, Kentucky, umepiga kura kwa wingi wa asilimia 70 ukiunga mkono azimio la kuitangaza Israeli kama dola la ubaguzi wa rangi.
-
Mahujaji wa Kiirani walaani kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel
Jul 09, 2022 05:15Ummati mkubwa wa Mahujaji wa Kiirani sambamba na kutangaza uungaji mkono wao kwa wananchi wa Palestina, lakini umekosoa pia njama ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Makundi ya muqawama Palestina yamkosoa Abbas kukutana na Gantz
Jul 09, 2022 03:05Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina Mahmoud Abbas amekosolewa vikali na makundi ya muqawama ya Palestina, kwa kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel, Benny Gantz.
-
UN: Kufukuzwa Wapalestina eneo la Masafer Yatta ni jinai ya kivita
Jul 08, 2022 03:41Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu (OCHA) imetangaza kuwa kufukuzwa kwa Wapalestina kutoka eneo la Masafer Yatta, kusini mwa Ukingo wa Magharibi, kunaweza kuwa sawa na kuwalazimika kuyahama makazi yao, jambo ambalo ni ukiukaji mkubwa wa Mkataba wa Nne wa Geneva na hivyo kuzingatiwa kuwa ni uhalifu wa kivita.
-
Raisi: Uwepo wa utawala wa Kizayuni unadhoofisha usalama wa eneo
Jun 29, 2022 22:24Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uwepo wa utawala wa Kizayuni wa Israel unaibua taharuki na kudhoofisha usalama wa eneo hili la Asia Magharibi.
-
Onyo la Mkuu wa Kamandi ya Majeshi ya Iran kwa Israel
Jun 27, 2022 06:55Kamanda mkuu wa vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameuonya vikali utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya kuchukua hatua yoyote ya kichokozi katika eneo la Asia Magharibi na kusisitiza kuwa, sera ya Israel ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine na chokochoko zozote za utawala huo katika eneo zitakabiliwa na jibu mwafaka.
-
Ripoti: Wazayuni wamewaua shahidi watoto 15 wa Kipalestina
Jun 27, 2022 06:51Ripoti mpya ya shirika moja la kutetea haki za watoto imesema askari makatili wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi kwa kuwapiga risasi watoto 15 wa Palestina.
-
NYT: Risasi iliyomuua Shireen Abu Akleh ilifyatuliwa na askari wa Kikosi cha Maalumu cha Israeli
Jun 20, 2022 22:09Uchunguzi mpya wa gazeti la Marekani la New York Times umethibitisha kuwa risasi iliyomuua mwandishi wa habari wa televisheni ya Al Jazeera ya Qatar, Shireen Abu Akleh, ilifyatuliwa na mwanajeshi wa kikosi maalumu cha Israel, katika eneo ambalo halikuwa na mwanamgambo hata mmoja wa Kipalestina.
-
Iraq yatakiwa kuchunguza wizi wa mafuta yanayopelekwa Israel
Jun 18, 2022 06:58Serikali ya Iraq imetakiwa ifanye uchunguzi wa kina kuhusu wizi wa mafuta ya nchi hiyo katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Kurdistan, kaskazini mwa nchi na kupelekwa katika ardhi za Wapalestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel.
-
Wapalestina 3 wauawa shahidi na jeshi la Israel mjini Jenin
Jun 17, 2022 06:56Jeshi katili la utawala haramu wa Israel limewaua shahidi vijana watatu wa Kipalestina katika mji wa Jenin, kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.