-
Wabunge Amerika ya Latini wataka kususiwa utawala wa Kizayuni
Sep 07, 2020 22:06Wabunge wa baadhi ya nchi za Amerika ya Latini wametaka kutungwe sheria za kuususia na kuuwekea vikwazo utawala wa Kizayuni wa Israel kutokana na mpango wa utawala huo ghasibu wa kutaka kuteka ardhi zaidi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Malalamiko ya Sudan kuhusu mashinikizo ya Marekani ya kuwa na uhusiano na Israel
Sep 06, 2020 07:12Serikali ya Trump muda wote imekuwa ikijionesha ni mtumishi asiye na doa wa malengo ya utawala wa Israel na imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kama kuzilazimisha nchi za Kiarabu na za Waislamu kutangaza uhusiano wa kawaida na utawala huo wa Kizayuni. Hata hivyo baadhi ya nchi kama Sudan zimeamua kupinga na pia kukabiliana na njama hizo.
-
Imarati kufungua ubalozi wake Israel ndani ya miezi 5
Sep 05, 2020 06:53Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Falme za Kiarabu amesema nchi hiyo inatazamiwa kufungua ubalozi ndani ya utawala haramu wa Israel katika kipindi cha kati ya miezi mitatu hadi mitano.
-
Netanyahu: Tunafanya mazungumzo ya siri na nchi nyingi za Kiarabu
Aug 31, 2020 08:11Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel amesema Tel Aviv hivi sasa inafanya mazungumzo ya siri na viongozi wengine wengi wa nchi za Kiarabu, juu ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na nchi hizo.
-
Nasrullah: Kuanzisha uhusiano na Israel ni huduma ya bwerere kwa Netanyahu na Trump
Aug 30, 2020 22:04Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amekosoa vikali hatua ya Umoja wa Falme za Kiarabu ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel na kubainisha kuwa: Kitendo hicho cha Abu Dhabi ni huduma bila malipo kwa watawala wa Marekani na Israel wanaoadamwa na misukosuko ya kisiasa.
-
Imarati yazidi kuikumbatia Israel, yaruhusu ndege za utawala huo
Aug 29, 2020 19:28Umoja wa Falme za Kiarabu umebatilisha sheria ya kuususia utawala haramu wa Israel na adhabu ya kukiuka sheria hiyo iliyokuwa imepiga marufuku kufanya miamala yoyote ya kibiashara na kifedha na utawala huo wa Kizayuni.
-
Iran: 'Mashariki ya Kati' mpya itaanzishwa kwa kutimuliwa Marekani katika eneo
Aug 28, 2020 08:05Msaidizi maalumu wa Spika wa Bunge la Iran katika masuala ya kimataifa amesema: 'Mashariki ya Kati' mpya itaundwa baada ya kuhakikisha Marekani imeshatimuliwa kikamilifu katika eneo hili la Asia Magharibi.
-
Safari ya Mike Pompeo kusini mwa Ghuba ya Uajemi na kukaririwa madai yasiyo na msingi wowote
Aug 28, 2020 01:59Marekani daima ikiwa na lengo la kuendeleza uwepo wake wa kijiopolitiki katika eneo la Ghuba ya Uajemi imekuwa ikitumia vizingizio visivyokuwa na maana hususan kupiga kwake ngoma ya kueneza chuki chidi ya Iran.
-
Safari ya Mike Pompeo nchini Sudan; juhudi za kuanzishwa uhusiano kati ya Khartoum na Tel-Aviv
Aug 27, 2020 03:10Licha ya juhudi za Mike Pompeo, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani za kuifanya Sudan ikubali kuanzisha uhusiano rasmi wa kidiplomasia na utawala haramu wa Israel, lakini Abdalla Hamdok, Waziri Mkuu wa serikali ya muda ya Sudan amesisitiza kuwa, hana mamlaka ya kuchukua maamuzi kuhusiana na uhusiano na Israel.
-
Safari ya kieneo ya Mike Pompeo; juhudi za kuupa uhalali utawala wa Kizayuni wa Israel
Aug 25, 2020 07:49Katika kipindi cha uongozi wa Rais Donal Trump nchini Marekani, nchi hiyo imefanya mambo na kuchukua hatua ambazo hazijawahi kushuhudiwa huko nyuma kwa maslahi ya utawala haramu wa Israel.