-
Shambulizi la anga la Israel laua shahidi Wapalestina 4 Gaza
Aug 25, 2020 03:28Wapalestina wanne wameuawa shahidi baada ya ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel kushambulia kwa mabomu maeneo kadhaa ya Palestina huko mashariki mwa Ukanda wa Gaza.
-
Algeria: Kuitetea na kuiunga mkono Palestina ni katika sera zetu za nje
Aug 24, 2020 23:01Msemaji wa serikali ya Algeria amesema kusimama na wananchi wa Palestina, kuwatetea na kuwaunga mkono nio katika sera za nje zilizopewa kipaumbele na taifa hilo la Kiarabu la kaskazini mwa Afrika.
-
Maulamaa wa Kisunni Iran walaani makubaliano ya Israel na UAE
Aug 24, 2020 07:31Wanazuoni wa Kisunni hapa nchini Iran wamekosoa vikali mapatano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya pande mbili hizo.
-
Hizbullah ya Lebanon yatungua ndege ya kijasusi ya Israel
Aug 24, 2020 07:26Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imefanikiwa kutungua ndege isiyo na rubani ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel
-
Sheikh Naim Qassim: Hizbullah haitoruhusu Israel iivamie Lebanon
Aug 22, 2020 03:12Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, harakati hiyo ya Kiislamu kamwe haitoiruhusu Israel na waungaji mkono wake waivamie tena Lebanon.
-
Baraza la Taasisi za Kiislamu Marekani lapinga mapatano ya fedheha kati ya Imarati na Israel
Aug 15, 2020 02:15Baraza la Taasisi za Kiislamu za nchini Marekani (USCMO) limepinga mpango wa mapatano uliofikiwa kati ya Imarati na Israel.
-
Iran yapinga kimya cha wakala wa IAEA kuhusu shughuli za nyuklia za Saudia
Aug 14, 2020 22:29Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Geneva amepinga kimya cha Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) kuhusu shughuli za siri za nyuklia za Saudi Arabia na silaha za nyuklia za utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Muungano wa Maulama wa Kiislamu: Hatua ya Imarati kuanzisha uhusiano na Israel ni usaliti mkubwa
Aug 14, 2020 22:28Jumuiya ya Muungano wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu imelaani makubaliano ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Imarati na utawala haramu wa Israel yaliyofikiwa kwa upatanishi wa Marekani.
-
Rashida Tlaib: Waislamu hawatahadaiwa na mapatano ya Trump na Netanyahu
Aug 14, 2020 05:22Mbunge Mwislamu wa Kongresi ya Marekani, Rashida Tlaib, amepinga vikali hatua ya Imarati ya kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema kuwa: Waislamu hawatahadaiwa na mapatano ya Rais Donald Trump wa Marekani na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.
-
'Israel' inaongoza kwa maambukizi ya corona duniani
Aug 06, 2020 21:55Mkuu wa kupambana na ugonjwa wa corona au COVID-19 katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) amesema: "Kwa kuzingatia idadi ya watu, Israel inaongoza kwa kuwa maambukizi ya juu zaidi ya corona duniani."