-
Rouhani: Jamii ya kimataifa inapaswa kukomesha jinai za Israel dhidi ya Wapalestina
May 14, 2020 19:59Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema jamii ya kimataifa ina wajibu wa kuchukua hatua za kivitendo za kukomesha jinai dhidi ya binadamu, ukandamizaji na dhulma wanazofanyiwa Wapalestina na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Amnesty yaikosoa Marekani kwa kuungo mkono uporaji wa ardhi za Wapalestina
May 14, 2020 19:58Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limekosoa vikali hatua ya Marekani ya kuunga mkono uamuzi wa utawala wa Kizayuni wa kulinyakua eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuliunganisha na ardhi zingine unazozikalia kwa mabavu za Palestina (Israel).
-
Ziara ya Pompeo katika ardhi za Palestina na malengo yake kadhaa
May 13, 2020 23:20Uhusiano wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel umepanuka sana kwa namna ambayo haijawahi kutokea katika wakati huu wa urais wa Donald Trump huko Marekani ambaye amechukua hatua nyingi za kutekeleza kivitendo matakwa haramu ya 'Israel.'
-
Bunge la Iran lapasisha muswada wa kukabili njama za Israel
May 12, 2020 10:22Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) imepasisha kwa kauli moja muswada wa dharura wa kukabili njama za utawala wa Kizayuni wa Israel, dhidi ya amani na usalama wa kieneo na kimataifa.
-
Vyama vya siasa na mashirika ya Norway yataka kuhitimishwa mzingiro wa Gaza
May 10, 2020 19:53Vyama vya kisiasa na mashirika 58 ya Norway yametoa mwito wa kufutwa haraka mzingiro wa Israel dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza, hususan katika kipindi hiki cha janga la corona.
-
Haniyah: Kuufanya wa kawaida uhusiano na Israel ni kosa lisilosameheka
May 09, 2020 08:03Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema njama zozote zinazolenga kuufanya wa kawaida uhusiano baina ya mataifa ya Kiarabu na utawala haramu wa Israel ni kosa ambalo halina msahama.
-
HAMAS na Jihadul Islami zapinga mpango wa kufanya mazungumzo na Israel
May 08, 2020 03:45Harakati za Muqawama wa Kiislamu za Palestina HAMAS na Jihadul-Islami zimekosoa vikali mpango wa baadhi ya nchi za Kiarabu wa kutaka kurejea kwenye meza ya mazungumzo na utawala haramu wa Israel.
-
HAMAS yatahadharisha kuhusu njama za kuiyahudisha Palestina
May 07, 2020 03:23Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeutaja mpango wa kuunganisha Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel) kama njama hatari zaidi ya kuziyahudisha ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Nasrullah: Tangazo la Ujerumani dhidi ya Hizbullah ni kwa maslahi ya Wazayuni
May 04, 2020 22:18Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon sanjari na kulaani hatua ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ujerumani ya kuiita harakati hiyo ya muqawama kuwa ni kundi la kigaidi, amesisitiza kuwa serikali ya Berlin imeshindwa kuwasilisha ithibati yoyote ya kuyapa nguvu madai yake hayo.
-
Hamas yatungua 'drone' ya jeshi la Israel Ukanda wa Gaza
Apr 28, 2020 02:44Harakati ya muqawama wa Kiislamu ya Palestina (Hamas) imefanikiwa kutungua ndege isiyo na rubani ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.