-
Baraza Kuu la UN; uwanja wa kukejeliwa Trump, jukwaa la mazingaombwe ya Netanyahu
Sep 28, 2018 10:44Kikao cha kila mwaka cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kimefanyika, huku walimwengu wakijionea igizo jengine la usanii wa Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel; utawala ambao una mamia ya vichwa vya nyuklia, silaha ambazo ni tishio na hatari kwa usalama wa dunia. Hata hivyo kutokana na kuungwa mkono na Marekani, utawala huo khabithi hauwajibiki kwa taasisi yoyote ile duniani.
-
Iran: Israel itajuta kwa kuwaunga mkono magaidi na kuishambulia Syria
Sep 27, 2018 12:39Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran ameuonya vikali utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya kuendelea kuzishambulia ngome za jeshi la Syria na waitifaki wake na kusisitiza kuwa, Tel Aviv itakabiliwa na jibu kali iwapo haitasitisha uvamizi wake na kuyaunga mkono makundi ya kigaidi katika nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Wanaharakati Misri watoa wito wa kukabiliana na kanali 27 za satalaiti za TV za Kiarabu zinazoanzishwa na Israel
Sep 27, 2018 12:17Wanaharakati nchini Misri wametaka zichukuliwe hatua kukabiliana na kampeni inayofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha kanali za televisheni za satalaiti za lugha ya Kiarabu.
-
Answarullah yakosoa vikali uhusiano wa Saudia na Israel; yasema tutaendelea kuwaunga mkono Wapalestina
Sep 27, 2018 03:55Msemaji wa harakati ya Answarullah ya nchini Yemen amekosoa vikali kitendo cha viongozi wa Saudia, Imarati na Bahrain cha kuonana na mkuu wa shirika la kijasusi la Israel huko New York Marekani na kusisitiza kuwa, wananchi wa Yemen hawatowaacha mkono kamwe ndugu zao Wapalestina.
-
Afrika Kusini yakanusha taarifa za kurejea tena balozi wake mjini Tel Aviv
Sep 26, 2018 23:30Serikali ya Afrika Kusini imekanusha taarifa zilizoenea kwamba, imemrejesha huko Tel Aviv balozi wake ambaye ilimwita nyumbani mwezi Mei mwaka huu.
-
Chama cha Labour: Uingereza iache kuiuzia silaha Israel
Sep 26, 2018 04:52Chama cha Labour cha nchini Uingereza kimeitaka serikali ya nchi hiyo kuacha kuuzia silaha utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Udharura wa kulazimishwa Israel kujiunga na mkataba wa nyuklia wa NPT
Sep 22, 2018 03:58Katika Mkutano Mkuu la 62 la Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki, kumesisitiziwa wajibu na udharura wa kulazimishwa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kujiunga na Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Silaha za Nyuklia, NPT.
-
Sayyid Hassan Nasrullah: Mashambulizi ya Israel nchini Syria hayavumiliki tena
Sep 19, 2018 23:22Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, mashambulizi ya mara kwa mara ya utawala wa Kizayuni wa Israel nchini Syria hayavumiliki tena na inabidi yakomeshwe.
-
Ismail Hania: Maandamano ya Haki ya Kurejea na kuondolewa mzingiro hayatasimama
Sep 19, 2018 10:14Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS amesisitiza kuwa, taifa la Palestina limeazimia kwamba, litasimama kidete kukabiliana na mzingiro wa adui Mzayuni hadi pale litakapousambaratisha.
-
Msimamo wa Theresa May wa kuitetea Israel, harakati ya kufuata nyayo za Trump
Sep 19, 2018 02:06Serikali ya Kihafidhina (Conservative) ya Uingereza inahesabiwa kuwa miongoni mwa watetezi na waungaji mkono wakubwa wa utawala wa Kizayuni wa Israel na licha ya jinai na uhalifu mkubwa unaofanywa na utawala huo dhidi ya watu wa Palestina, lakini hakushuhudiwi mabadiliko ya aina yoyote katika mienendo ya London katika uwanja huu.