-
UAE ilitumia spyware ya Israel kuwafanyia ujasusi viongozi wa eneo
Sep 01, 2018 09:33Utawala wa Umoja wa Falme za Kiarabu ulitumia programu ya kijasusi ya kudukua kompyuta au simu za mkononi (spyware) kuwafanyia ujasusi viongozi kadhaa wa nchi za Kiarabu akiwemo Amir wa Qatar, Waziri Mkuu wa Lebanon na mwanamfalme mmoja wa Saudia.
-
Zarif atoa jibu makini kwa vitisho vya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni dhidi ya Iran
Aug 30, 2018 03:04Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, vitisho vya waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kitendo kilichovuka mpaka wa utovu wa haya katika ulimwengu wa ufidhuli.
-
Taarifa ya HAMAS kwa mnasaba wa mwaka wa 49 tokea kuchomwa moto Msikiti wa al-Aqswa
Aug 21, 2018 21:47Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesisitiza kuwa, Wapalestina wataendeleza mapambano yao dhidi ya utawala ghasibu wa Israel yenye lengo la kukombolewa msikiti mtakatifu wa al-Aqswa.
-
UN yatoa mapendekezo ya kuboresha hali ya Wapalestina
Aug 18, 2018 10:00Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa mapendekezo kadhaa ya kuwasaidia watu wa Palestina katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na Israel.
-
Onyo la maafisa wa zamani wa kijasusi wa Marekani kuhusu nyaraka bandia za Netanyahu dhidi ya Iran
Aug 07, 2018 01:45Israel ambayo inahesabiwa kuwa mmoja wa maadui wakubwa wa Iran katika eneo la Mashariki ya Kati daima inafanya njama na kueneza madai ya uongo dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu hususan katika mradi wake wa amani wa nyuklia lengo lake kuu likiwa ni kutaka kupoteza imani ya jamii ya kimataifa na kuifanya ichukue hatua dhidi ya Iran.
-
Israel yaizuia boti ya pili ya shehena ya misaada iliyokuwa ikielekea Gaza
Aug 04, 2018 10:46Askari wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel wameizuia boti ya pili iliyokuwa imebeba shehena ya misaada ya kibinadamu kwa ajili ya Wapalestina wa eneo la Ukanda wa Gaza lililozingirwa na utawala huo.
-
Vita vya fueli vya Israel dhidi ya Gaza katikati ya msimu wa joto kali
Aug 03, 2018 02:33Avigdor Lieberman, Waziri wa Vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel ameliamuru jeshi la utawala huo lizuie kupelekwa fueli eneo la Ukanda wa Gaza.
-
Asilimia 92 ya Waarabu wanaiona Israel tishio kubwa zaidi kwa amani ya Mashariki ya Kati
Aug 01, 2018 21:59Uchunguzi wa maoni uliofanywa hivi karibuni katika Ulimwengu wa Kiarabu unaonyesha kuwa, kutokana na mtazamo hasi ulioko dhidi ya hamu ya baadhi ya nchi ya kutaka kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel, akthari ya wananchi katika nchi za Kiarabu wanauona utawala huo wa Kizayuni tishio kubwa zaidi kwa amani na uthabiti wa Mashariki ya Kati.
-
Jibu la Wapalestina kwa uharamia wa Israel
Aug 01, 2018 01:41Mkuu wa Idara ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) Ismail Hania ametoa ujumbe akilaani shambulizi la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya meli iliyokuwa njiani ikielekea Ukanda wa Gaza kuvunja mzingiro wa Israel dhidi ya wakazi wa eneo hilo na vilevile uharamia wa askari wa Israel wa kuwashambulia wanaharakati wa kimataifa wanaolitetea taifa la Palestina.
-
Palestina yateuliwa kuongoza Kundi la 77 la UN
Jul 27, 2018 03:36Palestina imeteuliwa kuwa mwenyekiti wa kiduru wa Kundi la 77 (G77) linalojihusisha na masuala ya uchumi wa nchi zinazostawi, ambazo zinaunda asilimia 80 ya idadi ya watu wote duniani.