-
Palestina yateuliwa kuongoza Kundi la 77 la UN
Jul 27, 2018 03:36Palestina imeteuliwa kuwa mwenyekiti wa kiduru wa Kundi la 77 (G77) linalojihusisha na masuala ya uchumi wa nchi zinazostawi, ambazo zinaunda asilimia 80 ya idadi ya watu wote duniani.
-
Fawzi Barhoum: Kunyamazia mashambulio ya Israel ni jambo lisilokubalika
Jul 26, 2018 09:55Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema kuwa, kunyamazia kimya hujuma na mashambulio ya utawala unaomwaga damu na unaotenda jinai wa Israel ni jambo lisilokubalika.
-
Jeshi la Israel lashambulia Gaza, Wapalestina 3 wauawa shahidi
Jul 26, 2018 02:43Kwa akali Wapalestina watatu wameuawa shahidi katika wimbi jipya la mashambulizi ya angani na nchi kavu ya jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya makazi ya raia katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel yabomoa kituo cha watoto wa Kipalestina mashariki wa mji wa Quds
Jul 25, 2018 22:36Duru za habari kutoka Palestina zimeripoti kwamba maboldoza ya utawala haramu wa Kizayuni, yamebomoa kituo cha kulelea watoto wadogo pamoja na kituo cha wanawake katika eneo la Jabal al Baba karibu na mji wa al-Eizariya, mashariki mwa mji wa Quds.
-
Erdogan: Israel ndio utawala wa kifashisti na kibaguzi zaidi duniani
Jul 24, 2018 11:50Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki ameutaja utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa ndio utawala wa kifashisti na wa kibaguzi zaidi duniani.
-
Indhari ya Umoja wa Mataifa kuhusiana na hali inayotia wasiwasi ya Ukanda wa Gaza
Jul 24, 2018 07:03Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, hali ya Ukanda wa Gaza ni ya "maafa" na ametahadharisha kwamba, hali hiyo itazidi kuwa mbaya.
-
Makamanda wa makundi ya kigaidi nchini Syria wakimbilia upande wa jeshi la Israel
Jul 23, 2018 22:53Sambamba na jeshi la Syria kuimarisha mzingiro dhidi ya makundi ya kigaidi kusini mwa nchi hiyo, makamanda wa makundi hayo na kupitia taa ya kijani ya utawala wa Kizayuni, wamekimbilia upande wa jeshi la Israel katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
Shakhsia wa Kiafrika: Israel isiruhusiwe kujipenyeza Afrika
Jul 22, 2018 23:12Shakhsia mbalimbali walioshiriki Kongamano la Kuiunga Mkono Palestina katika mji mkuu wa Mauritania, Nouakchott wamesisizia udharura wa nchi za Afrika kutouruhusu utawala wa Kizayuni wa Israel kujipenyeza katika bara hilo; na badala yake ziliunge mkono taifa la Palestina.
-
UN yaitaka Israel isitishe uchokozi wake Ghaza
Jul 22, 2018 03:10Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameutaka utawala haramu wa Israel usitishe uchokozi wake katika Ukanda wa Ghaza.
-
Mossad yakiri kushirikiana na kundi la kigaidi la MKO kula njama dhidi ya Iran
Jul 20, 2018 09:40Shirika la Ujasusi la Utawala wa Kizayuni wa Israel MOSSAD limejitokeza hadharani na kukiri kuhusu ushirikiano wake na kundi la kigaidi la MKO, kupanga njama dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.