-
Pezeshkian: Migawanyiko kati ya mataifa ya Kiislamu inainufaisha Israel pekee
Aug 25, 2025 07:30Rais wa Iran amesema umoja wa wananchi wa Iran na katika mataifa yote ya Kiislamu ndiyo kinga kuu dhidi ya vitisho vya maadui, akionya kuwa migawanyiko ni kwa maslahi ya Israel pekee.
-
Tangu Agosti 6, jeshi la Israel limebomoa kikamilifu majengo zaidi ya 1,000 ya Mji wa Ghaza
Aug 25, 2025 03:29Shirika la Ulinzi wa Raia la Palestina limetangaza kuwa jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limebomoa kikamilifu majengo zaidi ya 1,000 katika vitongoji vya Zeitoun na Sabra katika Mji wa Ghaza tangu lilipoanza kuuvamia mji huo mnamo Agosti 6, na hivyo kupelekea mamia ya Wapalestina kunasa chini ya vifusi vya majengo hayo.
-
Hamas yapongeza 'ujasiri' wa mawaziri wa Uholanzi kujiuzulu juu ya Gaza
Aug 24, 2025 23:27Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imepongeza hatua ya kujiuzulu mawaziri kadhaa wa Uholanzi, akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo, Caspar Veldkamp, kujibu hatua ya kukataa kwa serikali yao kuiwekea vikwazo Israel. Hamas imetaja kujiuzulu huko kama uamuzi wa kijasiri na wa kimaadili.
-
Jaribio la Wazayuni la kumuua kigaidi Mkuu wa Majeshi ya Yemen lagonga mwamba
Aug 24, 2025 23:00Vyombo vya habari vya Kizayuni vimeripoti habari ya kufeli jaribio la utawala haramu wa Israel la kumuua Mkuu wa Majeshi ya Yemen, kwa mara ya pili sasa.
-
Kashfa kubwa ya utawala wa Kizayuni: Israel, kituo kikubwa zaidi cha biashara ya dawa za kulevya barani Ulaya
Aug 23, 2025 06:09Kwa mujibu wa ripoti ya kituo cha runinga cha Israel, Channel 12, Israel inazidi kuwa kitovu kikuu cha biashara ya dawa za kulevya kuelekea katika nchi za Ulaya.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uholanzi ajiuzulu, kisa mkwamo wa vikwazo dhidi ya Israel
Aug 23, 2025 03:32Waziri wa Mambo ya Nje wa Uholanzi, Caspar Veldkamp amejiuzulu baada ya kushindwa kupata uungwaji mkono wa baraza la mawaziri kwa vikwazo zaidi dhidi ya Israel, kutokana na mashambulizi ya kijeshi ya utawala huo wa Kizayuni huko Gaza.
-
Jibu la Tunisia kwa kauli ya Netanyahu ni ishara ya wasiwasi wa nchi za Kiarabu kuhusu mipango ya upanuzi ya Israel
Aug 21, 2025 22:43Wananchi wa Tunisia wamefanya maandamano ya kupinga uzayuni wakilaani matamshi ya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu, kuhusu kile kinachoitwa “Israeli Kubwa.”
-
Hamas yaonya: Israel haitafikia malengo yake Ukanda wa Gaza
Aug 21, 2025 03:01Utawala wa Israel umeanza kupeleka vikosi vya jeshi lake kwenye viunga vya Jiji la Gaza kwa ajili ya kuanza kutekeleza mpango wake wa kukalia kwa mabavu eneo hilo kubwa zaidi la Ukanda wa Gaza, lakini Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeonya kuwa, Tel Aviv itashindwa kutimiza malengo yake.
-
Kwa nini utawala wa kizayuni wa Israel unataka kuzidisha satua na ushawishi wake barani Afrika?
Aug 20, 2025 23:29Katika mwendelezo wa hatua za kujaribu kuwa na satua na ushawishi katika nchi za Kiafrika, waziri wa mambo ya nje wa utawala wa kizayuni wa Israel Gideon Saar siku ya Jumanne alielekea Zambia katika safari ya kidiplomasia barani Afrika, madhumuni makuu yakiwa ni kufungua ubalozi wa utawala huo haramu nchini humo.
-
Ripoti: Israel imepatwa na mshtuko wa kiuchumi wa vita na Iran
Aug 19, 2025 08:04Ripoti ya vyombo vya habari vya Israel imefichua changamoto zinazoukabili utawala huo baada ya vita vya siku 12 na Iran mwezi Juni mwaka huu,na kubainisha kuwa uchumi wa Israel umedorora sana, na kushuka kwa viashiria vya jumla, ikiwa ni pamoja na kupungua kwa pato la taifa (GDP), uwezo wa manunuzi na uwekezaji.