-
Iran: Marekani ni mshirika wa jinai za Israel dhidi ya Wapalestina wa Gaza
Oct 25, 2023 04:07Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Marekani ni mshirika katika jinai za kutisha za Israel huko Ukanda wa Gazal kutokana na uungaji mkono wake usio na kifani kwa utawala huo unaokalia kwa mabavu ardhi za Palestina.
-
Muswada wa kujinaisha uhusiano na Israel wavuka kiunzi cha kwanza Tunisia
Oct 25, 2023 04:06Kamati ya Bunge la Tunisia imepasisha katika marhala ya kwanza muswada wa sheria inayotaka vitendo vya kuanzishwa uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Israel kuwa kosa la jinai.
-
Israel yafyata mkia, yasema haitaki kuingia vitani na Hizbullah
Oct 25, 2023 04:06Rais Isaac Herzog wa Israel amedai kuwa, utawala huo wa Kizayuni hauna azma ya kuingia vitani na Harakati ya Hizbullah ya nchini Lebanon katika upande wa kaskazini, siku chache baada ya viongozi wa Marekani kuwatahadharisha watawala wa Israel kuhusu ugumu na hatari ya kuendesha vita viwili kwa wakati mmoja; upande wa kusini na Harakati ya Hamas ya Palestina na upande wa kaskazini na harakati yenye nguvu kubwa ya kijeshi, Hizbullah.
-
Wadukuzi wa Algeria washambulia mitandao ya Wizara ya Vita ya Israel
Oct 24, 2023 23:22Kundi moja la wadukuzi la Algeria limejipenyeza na kushambulia mitandao ya kuhifadhi taarifa za Wizara ya Vita ya utawala haramu wa Israel.
-
Ajuza Muisrael aliyekuwa mateka asimulia alivyokirimiwa na wapiganaji wa HAMAS+VIDEO
Oct 24, 2023 11:02Mwanamke mzee Muisrael aliyeachiliwa huru na wapiganaji wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema alikirimiwa na kutendewa wema katika muda wa wiki mbili alipokuwa ameshikiliwa mateka na kundi hilo la wanamapambano wa Palestina.
-
Amir wa Qatar: Dunia isiipe Israel leseni ya kuwaua Wapalestina
Oct 24, 2023 10:24Amir wa Qatar amesema anatiwa wasiwasi na hatua ya Israel ya kushadidisha jinai na mashambulizi katika Ukanda wa Gaza huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kuiasa jamii ya kimataifa isiupe leseni utawala huo wa Kizayuni ya kuwaua shahidi wananchi wa Palestina.
-
Upinzani mkali wa Marekani dhidi ya juhudi za kusitisha vita Ghaza
Oct 24, 2023 06:33Marekani ikiwa ni mshirika wa kistratijia wa utawala wa Kizayuni si tu kwamba inatoa misaada ya kila aina ya silaha na fedha kwa ajili ya kuushambuliwa Ukanda wa Ghaza, bali pia inapinga vikali usitishwaji vita katika uvamizi huo wa umwagaji damu kwa visingizio vya uongo na visivyo na msingi.
-
Gaza: Israel imevunja kabisa misikiti 31 na kuharibu vibaya makanisa 3
Oct 22, 2023 11:27Ofisi ya Vyombo ya Habari vya Serikali ya Ukanda wa Gaza imetangaza leo Jumapili kwamba idadi ya misikiti iliyovunjwa kabisa katika mashambulizi ya jeshi la Israel katika Ukanda wa Gaza imeongezeka na kufikia misikiti 31, na uharibifu mkubwa umerekodiwa katika makanisa 3.
-
Hizbullah: Ukanda wa Gaza utakuwa kaburi la utawala wa Kizayuni
Oct 21, 2023 23:52Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya nchini Lebanon amesema jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza hazitapita hivi hivi bila kupatiwa jibu na kusisitiza kuwa, eneo hilo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu litageuka na kugeuka na kuwa kaburi la kuuzika utawala huo bandia.
-
Viongozi wa nchi za Kiarabu walaani mashambulizi ya Israel huko Gaza, wahimiza juhudi mpya za amani Palestina
Oct 21, 2023 23:50Viongozi wa nchi za Kiarabu wametoa wito wa kuanzishwa upya juhudi za amani kati ya Israel na Palestina ili kukomesha uvamizi wa Israel na kutatua mzozo unoendelea kwa miongo kadhaa kati ya pande hizo mbili, huku utawala haramu Israel ukiendeleza mashambulizi ya kikatili dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza.