-
Syria yalalamikia kushadidi jinai za Marekani
Mar 23, 2017 15:25Wizara ya Mambo ya Nje ya Syria katika kulalamikia jinai za muungano wa Marekani wa eti kupambana na magaidi wa ISIS au Daesh, imelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kutekeleza majukumu yake na kusitisha mauaji ya raia na uharibifu unaofanywa na muungano wa kimataifa unaoongozwa na Marekani nchini Syria.
-
Kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni na kutojali kwake ripoti za Umoja wa Mataifa
Mar 22, 2017 16:28Katika hali ambayo jinai na sera za kujipanua za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina zinakabiliwa na malalamiko na upinzani wa walimwengu pamoja na jumuiya za kimataifa, utawala huo dhalimu umeamua kushadidisha mashambulio yake dhidi ya wananchi hao madhulumu.
-
Radiamali ya Umoja wa Mataifa kwa hatua zilizo dhidi ya ubinadamu za utawala wa Israel
Feb 28, 2017 02:43Umoja wa Mataifa umetangaza katika ripoti yake kwamba, katika kipindi cha majuma mawili yaliyopita, utawala wa Kizayuni wa Israel umebomoa makumi ya nyumba za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na hivyo kuwaacha Wapalestina wengine wakitangatanga kutokana na kutokuwa na makazi.
-
Udharura wa kuundwa kamati ya kutafuta ukweli kuhusu jinai za kivita za Saudi Arabia
Feb 15, 2017 02:57Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Serikali ya Wokovu wa Kitaifa ya Yemen kwa mara nyingine tena sambamba na kumtaka Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa kufanya safari nchini Yemen ili ashuhudie kwa karibu hali ya nchi hiyo ameitaka taasisi hiyo ya kimataifa iunde kamati huru ya kutafuta ukweli.
-
Utendaji dhaifu wa Jamii ya Kimataifa kuhusiana na maafa ya kibinadamu nchini Yemen
Feb 03, 2017 04:21Umoja wa Mataifa umesema unatiwa wasiwasi na hali ya usalama ya raia wa Yemen katika miji ya Dhubab na Almakha iliyoko kwenye mkoa wa Taiz. Kuhusiana na suala hilo, Jamie McGoldrick, Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Yemen ametoa taarifa na kutangaza kuwa ripoti kutoka maeneo hayo zinaonyesha kwamba operesheni za kijeshi zilizofanywa kwenye maeneo ya pwani ya miji ya Dhubab na Almakha zimewafanya wakaazi wake walazimike kuzihama nyumba zao.
-
UN: Saudi Arabia imetenda jinai kubwa za kivita nchini Yemen
Jan 31, 2017 04:10Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, Saudi Arabia imefanya jinai za kivita katika mashambulizi yake ya kijeshi nchini Yemen.
-
Kuendelea jinai za Saudia nchini Yemen kunatokana na uzembe wa Umoja wa Mataifa
Jan 28, 2017 02:49Akizungumza siku ya Alkhamisi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Stephen O'Brien, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia Masuala ya Kibinadamu na Misaada ya Dharura amesisitiza kwamba ndege za kivita za Saudi Arabia zingali zinaendesha hujuma ya kuwaua ovyo na kwa umati raia wa nchi jirani ya Yemen.
-
Ukuta wa uzio katika mpaka wa Gaza; dharau ya Israel kwa Baraza la Usalama la UN
Jan 11, 2017 15:00Wakati Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio nambari 2234 la kuutaka utawala wa Kizayuni wa Israel usimamishe ujenzi wa vitongoji katika ardhi za Palestina unazozikalia kwa mabavu, waziri wa vita wa utawala huo haramu ameafiki shauri la kujengwa ukuta wa uzio katika mipaka ya Ukanda wa Gaza.
-
Jinai za kivita Syria na jukumu la Katibu Mkuu mpya wa UN
Jan 07, 2017 03:19Katika radiamali yake ya kwanza kabisa kuhusiana na mgogoro wa Syria katika kipindi cha katibu mkuu António Guterres, Umoja wa Mataifa umelaani kitendo cha magenge ya kigaidi cha kuwakatia maji wananchi wa Damascus Syria na kusema hiyo ni jinai ya kivita.
-
HRW: Silaha za Marekani zinatumiwa na Saudia kutenda jinai za kivita Yemen
Dec 03, 2016 04:25Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch kwa mara nyingine limetoa wito kwa Marekani kusitisha uuzaji wake wa silaha kwa Saudi Arabia.