-
Ongezeko la vyama vya siasa Kenya kabla ya uchaguzi wa 2027, mradi wa kibiashara?
Oct 29, 2023 10:50Ongezeko la vyama vya siasa vinavyojiandikisha nchini Kenya kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027 limetajwa kuwa ni mradi wa viongozi wa vyama hivyo kwa ajili ya kujipatia kitita kikubwa cha fedha za walipakodi wa Kenya.
-
Wakenya wawasha mishumaa kuonyesha mshikamano na Wapalestina
Oct 15, 2023 07:58Wananchi wa Kenya wamekusanyika na kuwawasha mishumaa katika mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi kuonyesha mshikamano wao na wananchi wa Palestina. Mashirika yaliyoandaa shughuli hiyo ni pamoja na Kenyans 4 Palestine, The Pan African Palestine Solidarity Network (PAPSN) na podkasti ya 'Until Everyone is Free.'
-
Waislamu Kenya wapinga hatua ya Mahakama ya Juu kuruhusu mashoga kusajiliwa
Sep 23, 2023 23:44Viongozi na wasomi wa dini ya Kiislamu wa Kenya wamelaani vikali uamuzi wa Mahakama ya Juu kuruhusu makundi ya mashoga na wasagaji kusajiliwa.
-
Rais wa Kenya: Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa halifai, libadilishwe
Sep 22, 2023 04:04Takwa la muda mrefu la viongozi wengi hususan kutoka Barani Afrika la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lililoundwa tarehe 25 Octoba mwaka 1945 kufanyiwa marekebisho makubwa limeendelea kuchukua nafasi katika hotuba za viongozi wa ngazi za juu wanaohutubia katika mkutano wa 78 wa Baraza Kuu la UN jijini New York ambapo Rais William Ruto wa Kenya amesema sababu zote za kulifanyia marekebisho baraza hilo zipo wazi.
-
Kenya kupeleka vikosi maalumu pwani na kaskazini kukabiliana na ukosefu wa usalama
Sep 20, 2023 23:05Serikali ya Kenya inapanga kupeleka vikosi maalumu katika maeneo ya kaskazini na pwani ili kukabiliana na tishio la ugaidi kufuatia ongezeko la mashambulizi ya kigaidi katika maeneo hayo.
-
Balozi wa Kenya nchini Iran atembelea viwanda vya uzalishaji Arak
Aug 21, 2023 07:39Balozi wa Kenya mjini Tehran ametembelea viwanda vya uzalishaji katika mji wa Arak, makao makuu ya mkoa wa Markazi, unaofahamika kama mji mkuu wa viwanda wa Iran.
-
Shambulio la kigaidi la Al-Shabaab laua watu wawili na kujeruhi wengine 10 Lamu, Kenya
Aug 02, 2023 04:27Watu wawili wameaga dunia na wengine wapatao 10 wamejeruhiwa, akiwemo diwani wa eneo moja wakati magaidi 60 wanaoshukiwa kuwa wanachama wa kundi la Al-Shabaab walipovamia magari katika eneo la Mwembeni, karibu na Lango la Simba kwenye barabara kuu ya Lamu-Witu-Garsen nchini Kenya.
-
Kenya yasema iko tayari kuongoza kikosi cha kimataifa cha kurejesha utulivu Haiti
Jul 30, 2023 23:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya Alfred Mutua amesema nchi yake iko tayari kuongoza kikosi cha kimataifa nchini Haiti; na itapeleka maafisa 1,000 wa polisi katika taifa hilo la Karibean lililokumbwa na mapigano mara tu pendekezo lake litakapokubaliwa.
-
Odinga alaani ukatili wa polisi, asema Ruto alikatiza juhudi za upatanishi za Rais Samia
Jul 25, 2023 11:50Kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Kenya, Raila Odinga leo Jumanne amelaani "ukatili usio na kifani wa polisi" wakati wa maandamano ya kupinga serikali na gharama za juu za maisha ambayo yamekuwa yakifanyika katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki katika miezi ya hivi karibuni.
-
Balozi wa Iran nchini Kenya: Jamhuri ya Kiislamu imefanikiwa kupanua ushirikiano na nchi za Afrika
Jul 14, 2023 04:32Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Kenya amesema kuwa utendaji wa Serikali ya Awamu ya 13 umekuwa na mafanikio katika kupanua ushirikiano na Kenya.