-
Rais Macron akabiliwa na upinzani baada ya matamshi yake makali kwenye mkutano wa Nairobi
May 13, 2026 12:14Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron anakabiliwa na upinzani mkali baada ya kukatiza kikao cha mjadala katika kongamano la Africa Forward Summit nchini Kenya akiwataka hadhirina wanyamaze kimya.
-
Kenya yataka Afrika ipewe kiti cha kudumu katika Baraza la Usalama la UN
May 12, 2026 14:25Rais wa Kenya, William Ruto, ametoa wito kwa Afrika kupewa uanachama wa kudumu katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, takwa ambalo limeungwa mkono na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.
-
UN kujenga ofisi mpya yenye thamani ya dola milioni 340 Nairobi
May 12, 2026 09:01Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amshuhudia uwekezaji mkubwa wa Umoja wa Mataifa wenye thamani ya karibu dola milioni 340 katika ofisi yake katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
-
Macron asema Ufaransa “haikuwahi kufikiria” kupeleka jeshi Hormuz bila uratibu na Iran
May 12, 2026 04:28Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amesema Paris haijawahi kufikiria kupeleka vikosi vya kijeshi vya Ufaransa katika Mlango-Bahari wa Hormuz bila uratibu na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wakati mvutano unaochochewa na vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran ukiendelea.
-
Polisi Kenya yathibitisha vifo vya watu 18 katika maporomoko ya ardhi
May 04, 2026 10:21Huduma ya Polisi ya Kenya Jumapili ilithibitisha kupoteza maisha watu 18 kufuatia maporomoko ya udongo na mafuriko huku mvua kubwa ikiendelea kunyesha katika maeneo kadhaa ya nchi hiyo, na kulazimisha familia nyingi kuhama makazi yao.
-
Kenya yaitaka Russia iirejeshee miili na raia wake waliofungwa katika vita vya Ukraine
Feb 21, 2026 07:37Serikali ya Kenya imeitaka Russia iirejeshe nyumbani miili ya raia wake waliouawa na wale waliokamatwa kama wafungwa wa vita, ambao wameripotiwa kuwa walipiigania Russia katika vita na Ukraine.
-
Russia yakanusha madai ya kuwaajiri Wakenya katika vita vya Ukraine
Feb 20, 2026 03:42Russia imekanusha madai kwamba inawaajiri Wakenya kupigana vitani nchini Ukraine, kufuatia ripoti za Huduma ya Kijasusi ya Kitaifa ya Kenya kwamba zaidi ya Wakenya 1,000 kwa sasa wanapigana upande wa Russia katika mzozo huo.
-
Balozi wa Iran aiasa Kenya kuchukua hatua 'sakata la chai'
Feb 18, 2026 03:53Mwanadiplomasia wa Iran imeiomba serikali ya Kenya kuchukua hatua na kulipatia ufumbuzi sakata la chai la thamani ya Shilingi bilioni 2.6 za nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
Wakenya: Mradi wa kilimo wa Israel Nakuru ni mwanzo wa unyakuzi wa ardhi zetu
Feb 17, 2026 02:52Mradi wa Israel wa kilimo na makazi wa ekari 520 huko Solai, Kaunti ya Nakuru nchini Kenya umezua mjadala mkali wa kitaifa. Wakenya wametumia mitandao ya kijamii kupinga mradi huo, wanaotaja kuwa mwanzo wa unyakuzi wa ardhi za nchi hiyo na utawala ghasibu wa Israel.
-
Serikali ya Kenya yamuongezea mchungaji Mackenzie mashtaka kwa vifo vya watu wengine 52
Feb 12, 2026 03:00Paul Mackenzie, kiongozi wa tapo la kikristo nchini Kenya aliyewaamuru wafuasi wake wajiue kwa njaa wao na watoto wao ili waende mbinguni amesomewa shtaka jengine jipya yeye na wenzake saba la kusababisha vifo vingine 52, kupitia mahubiri yake.