-
Polisi Kenya wamjeruhi vibaya kwa risasi kijana aliyetaka kuingia Ikulu kwa nguvu + Sauti
Jun 11, 2019 12:08Polisi nchini kenya wamempiga risasi na kumjeruhi vibaya jamaa mmoja aliyekua akijaribu kuingia katika ikulu ya rais jijini Nairobi huku akiwa amejihami kwa kisu mkononi. Seifullah Murtadha na maelezo zaidi kutoka Mombasa, Kenya.
-
Mkenya atakiwa aukane uraia wa Marekani kabla ya kuwa balozi
Jun 07, 2019 02:53Raia wa Kenya ambaye pia ana uraia wa Marekani ametakiwa aukane uraia wa Marekani kabla ya kuchukua nafasi ya balozi wa Kenya nchini Korea Kusini.
-
Kenya yazindua sarafu mpya Madaraka Day + Sauti
Jun 01, 2019 12:23Taifa la kenya limezindua sarafu mpya katika maadhimisho ya 56 ya Madaraka Day ili kupambana na ufisadi. Rais Uhuru Kenyatta amesema kuwa, pasi na kushirikiana ili kuukomesha ufisadi basi ndoto za waanzilishi wa taifa za kuona Kenya ni taifa lililostaarabika katika kila Nyanja, zitashindwa kutimia. Seifullah Murtadha na maelezo zaidi kutoka Mombasa, Kenya.
-
Kenya na Somalia zaendelea kuvutana, Mogadishu yafuta mikutano ya Nairobi
May 27, 2019 02:51Katika kile kinachoonekana ni kuendelea kushtadi mvutano kati ya Kenya na Somalia, serikali ya Mogadishu imejibu mapigo na kufuta mikutano yake iliyotazamiwa kufanyika jijini Nairobi.
-
Mahakama ya Kenya yaamuru wahajiri 22 wa Eritrea warudishwe kwao
May 25, 2019 03:46Mahakama nchini Kenya imeagiza raia 22 wa Eritrea waliokamatwa siku 10 zilizopita na kushtakiwa kwa kuwa nchini humo kinyume cha sheria warejeshwe nchini kwao.
-
SAUTI, Mahakama Kuu ya Kenya yatupilia mbali pingamizi la mabaradhuli la kutaka kuhalalishwa mahusiano ya jinsia moja
May 24, 2019 11:30Hatimaye Mahakama Kuu nchini Kenya imechukua uamuzi wa kupongezwa, baada ya kukataa kufuta kifungu cha 162 cha sheria za nchi hiyo kinachoharamisha na kupiga marufuku mahusiano ya jinsia moja (yaani ubaradhuli).
-
UNHCR, SUPKEM zazindua kampeni ya "Ramadhani kwa ajili ya elimu kwa wakimbizi"
May 02, 2019 09:55Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) kwa ushirikiano na Baraza Kuu la Waislamu nchini Kenya (SUPKEM) limezindua kampeni ya kuwasaidia maelfu ya vijana wakimbizi nchini humo wanaokosa elimu.
-
Ujumbe wa Siku ya Wafanyakazi (Mei Mosi) nchini Kenya + Sauti
May 01, 2019 11:28Jamii ya wafanyakazi nchini Kenya imeitaka serikali kumaliza tatizo la ufisadi ambalo limeshika kasi sana nchini. Hayo yametolewa na wafanyakazi hao katika sherehe za Siku ya Mfanyakazi Duniani Mei Mosi ambapo pamoja na mambo mengine wameitaka serikali ya Nairobi kuwaandalia mazingira salama ya kazi ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.
-
IEA: Kenya na Uganda zinatakatisha 'fedha chafu' za Sudan Kusini
Apr 21, 2019 23:00Ripoti ya Taasisi ya Masuala ya Uchumi IEA imefichua kuwa, Kenya na Uganda zimefeli kuzuia mzunguko wa pesa haramu zinazotoka katika nchi changa zaidi barani Afrika, Sudan Kusini.
-
'Al-Shabaab' yawateka nyara madaktari 2 wa Cuba nchini Kenya
Apr 12, 2019 10:30Watu waliojizatiti kwa silaha wanaosadikiwa kuwa wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab wamewateka nyara madaktari wawili wa Cuba katika mpaka wa Kenya na Somalia.