-
Al-Shabaab yaua askari polisi 5 wa Kenya kaunti ya Mandera
Mar 02, 2018 04:24Askari polisi watano wa Kenya wameuawa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab kushambulia kambi mbili za maafisa usalama katika mji wa Fino katika kaunti ya Mandera.
-
Twaweza: Masikini wanazidi kuwa masikini na matajiri kuwa matajiri zaidi Kenya
Mar 01, 2018 01:21Uchunguzi umeonyesha kwamba, maskini wamezidi kuwa maskini huku wale wenye uwezo wa kifedha wakiendelea kuwa matajiri zaidi nchini Kenya.
-
Serikali ya Kenya yaahidi kukomesha ugaidi unaovuruga elimu
Feb 28, 2018 13:00Serikali ya Kenya imetangaza kuwa imebuni mpango ambao utahakikisha kwamba shughuli za masomo hazitaathiriwa katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo hususan katika Kaunti ya Wajir kutokana na mashambulizi ya kigaidi ya kundi la al Shabab.
-
Ulimwengu wa Michezo, Feb 26
Feb 26, 2018 04:26Huu ni mkusanyiko wa matukio muhimu ya spoti yaliyojiri duniani ndani ya siku saba zilizopita...
-
Maisha nchini Kenya yatabiriwa kuendelea kuwa magumu kutokana na kuendelea hali ya ukame
Feb 16, 2018 01:21Gharama ya maisha kwa raia wa Kenya inatazamiwa kupanda zaidi kutokana na kurefuka kipindi cha kiangazi na ongezeko la bei za mahitaji muhimu ya kuzalisha bidhaa.
-
Iran yavunja rekodi katika uuzaji wa gesi ya LPG Afrika, Asia
Feb 10, 2018 13:07Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeweka rekodi mpya katika uuzaji wa gesi aina ya LPG katika nchi kadhaa za mabara ya Afrika na Asia ambapo iliuza tani 520,000 Januari mwaka huu hilo likiwa ni ongezeko la asilimai 39.4 kutoka mwezi uliotangulia.
-
Polisi Kenya yamkamata mbunge wa tatu aliyeshiriki hafla ya kujiapisha Odinga
Feb 03, 2018 12:16Polisi ya Kenya imemtia nguvuni kwa muda na kumsaili mbunge wa tatu wa kambi ya upinzani nchini humo kwa tuhuma ya kushiriki katika hafla ya kuapishwa kinara wa kambi ya upinzani Raila Odinga kuwa "kiongozi wa wananchi" badala ya Rais Uhuru Kenyatta wa nchi hiyo aliyeshinda uchaguzi wa Oktoba mwaka jana.
-
UN yaitaka serikali ya Kenya iheshimu uhuru wa vyombo vya habari
Feb 03, 2018 04:05Umoja wa Mataifa umeitaka serikali ya Kenya kuheshimu agizo la mahakama lililoitaka ibatilishe hatua yake ya kuzifungia televisheni tatu kupeperushaji matangazo baada ya stesheni hizo kurusha moja kwa moja hafla ya kuapishwa kiongozi wa upinzani wa nchi hiyo Raila Odinga.
-
AU,EU wamkosoa kinara wa upinzani Kenya, Odinga, kwa kujiapisha
Feb 03, 2018 01:20Kiongozi wa muungano wa upinzani nchini KenYa, Raila Odinga amelaaniwa vikali na Umoja wa Ulaya na Umoja wa Afrika kwa kujiapisha kama 'rais wa wananchi' Januari 30 na kusema hatua hiyo inakiuka utawala wa sheria.
-
Serikali ya Kenya yapuuza amri ya Mahakama; yaendelea kukata matangazo ya stesheni tatu za TV
Feb 02, 2018 04:34Urushaji matangazo wa vituo vitatu vya televisheni nchini Kenya umeendelea kusimamishwa licha ya amri ya Mahakama Kuu ya nchi hiyo kuiamuru serikali iondoe zuio hilo.