Pars Today
Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ametahadharisha kuwa ubeberu wa Marekani umeingia katika hatua hatarishi zaidi na unajaribu kufanya kila njia ili kuzusha mapigano na kuwasha moto wa vita duniani.
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un ameionya Marekani kuwa nchi yake itajibu vitisho vya atomiki kwa silaha za atomiki na makabiliano kwa makabiliano dhidi yake.
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un amesema hakuna tija itakayopatikana kwa kufanya mazungumzo yoyote yale na Marekani na akabainisha kuwa kwa upande mmoja Washington inazungumzia kufanya mazungumzo na kuanzisha uhusiano; na kwa upande mwingine inatoa vitisho vya operesheni za kijeshi dhidi ya nchi hiyo.
Kwa mara nyingine tena, Korea Kaskazini imefyatua makombora yake ya balestiki kuelekea upande wa Japan, kujibu chokochoko mpya za Marekani dhidi ya Pyongyang.
Korea Kaskazini imefyatua kombora lake la balestiki kuelekea upande wa Japan, na kupelekea kusitishwa kwa usafiri wa treni katika baadhi ya maeneo, huku Wajapani katika maeneo ya kaskazini wakitakiwa kujificha.
Korea Kaskazini imefyatua kombora la balestiki kwa mara ya tatu ndani ya wiki moja mara baada ya kumalizika ziara ya makamu wa rais wa Marekani Kamala Harris nchini Korea Kusini.
Hatua ya Korea Kaskazini ya kufanyia majaribio kombora lake jipya kuelekea upande wa Bahari ya Japan imepokewa kwa hisia kali na nchi mbili za Japan na Korea Kusini.
Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un ametia saini sheria ambayo kwa mujibu wake nchi hiyo sasa inatambuliwa rasmi kuwa ni dola lenye nguvu za kijeshi za nyuklia.
Kiongozi wa Korea Kaskazini amesema kamwe Pyongyang haitasalimisha silaha zake za nyuklia au kutumia suala la kuharibu silaha hizo za maangamizi kujadiliana na Marekani.
Korea Kusini imesema, si baidi kwa Korea Kaskazini kufanya jaribio la saba la nyuklia hapo kesho.