-
Dada wa Kiongozi wa Koreka Kaskazini amuita Biden 'mzee asiye na mustakabali'
Apr 30, 2023 02:10Korea Kaskazini imemtuhumu Rais wa Marekani Joe Biden kwamba hana akili timamu baada ya kutishia kuiangamiza nchi hiyo iwapo itafanya shambulio la nyuklia na kuishutumu Marekani kwa ilichokiita sera "zilizofurutu mpaka" na za "uhasama".
-
Korea Kaskazini yafanyia majaribio droni yenye uwezo wa kufanya shambulio la nyuklia baharini
Mar 25, 2023 02:19Korea Kaskazini imeifanyia majaribio ndege mpya isiyo na rubani ya droni inayoweza kufanya mashambulizi ya nyuklia chini ya maji, likiwa ni jibu la kukabiliana na mazoezi ya pamoja ya kijeshi ya Marekani na Korea Kusini.
-
Korea Kaskazini: Hatari ya kutokea vita vya nyuklia imebadilika kutoka nadharia na kuwa uhalisia
Mar 09, 2023 06:41Korea Kaskazini imeonya kuhusu kile ilichokitaja kama hatari "halisi" ya kutokea vita vya nyuklia katika ukanda na dunia nzima, kufuatia duru mpya ya mazoezi ya pamoja ya kijeshi kati ya Korea Kusini na Marekani.
-
Korea Kaskazini yaonyesha makombora mapya ya kuvuka mabara ya ICBM
Feb 09, 2023 11:59Korea Kaskazini imeonyesha makombora yake mapya ya kisasa kabisa ya balestiki, yenye uwezo wa kuvuka mabara ya ICBM.
-
Korea Kaskazini kuongeza kiwango cha silaha za nyuklia kukabili tishio la US
Jan 01, 2023 07:19Kiongozi wa Korea Kaskazini ametoa amri ya kuzalishwa makombora mapya ya balestiki ya kuvuka mabara, sambamba na kuongezwa kiwango cha silaha za nyuklia za 'kimkakati' kwa ajili ya kukabiliana na tishio la Marekani.
-
Indhari ya Rais wa Venezuela kuhusu kufikia ubeberu wa Marekani katika hatua hatarishi zaidi
Dec 28, 2022 01:57Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ametahadharisha kuwa ubeberu wa Marekani umeingia katika hatua hatarishi zaidi na unajaribu kufanya kila njia ili kuzusha mapigano na kuwasha moto wa vita duniani.
-
Kiongozi wa Korea Kaskazini: Tutatumia silaha za atomiki kujibu vitisho vya atomiki
Nov 19, 2022 07:12Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un ameionya Marekani kuwa nchi yake itajibu vitisho vya atomiki kwa silaha za atomiki na makabiliano kwa makabiliano dhidi yake.
-
Kiongozi wa Korea Kaskazini: Hakuna faida ya kufanya mazungumzo na Marekani
Oct 11, 2022 07:23Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-Un amesema hakuna tija itakayopatikana kwa kufanya mazungumzo yoyote yale na Marekani na akabainisha kuwa kwa upande mmoja Washington inazungumzia kufanya mazungumzo na kuanzisha uhusiano; na kwa upande mwingine inatoa vitisho vya operesheni za kijeshi dhidi ya nchi hiyo.
-
Pyongyang yavurumisha tena makombora ya balestiki kujibu chokochoko za US
Oct 06, 2022 07:04Kwa mara nyingine tena, Korea Kaskazini imefyatua makombora yake ya balestiki kuelekea upande wa Japan, kujibu chokochoko mpya za Marekani dhidi ya Pyongyang.
-
Korea Kaskazini yafyatua kombora la balestiki kuelekea Japan
Oct 04, 2022 07:51Korea Kaskazini imefyatua kombora lake la balestiki kuelekea upande wa Japan, na kupelekea kusitishwa kwa usafiri wa treni katika baadhi ya maeneo, huku Wajapani katika maeneo ya kaskazini wakitakiwa kujificha.