-
Juhudi za kuweko mwafaka wa makundi ya kisiasa kwa ajili ya uchaguzi nchini Libya
Feb 23, 2023 02:32Katika hali ambayo Libya ingali inakabwa koo na jinamizi la mgogoro mkubwa wa kisiasa, mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika nchi hiyo ameyatolea mwito makundi ya kisiasa ya nchi hiyo kufikia mwafaka na kauli moja kuhusiana na kuitishwa uchaguzi mwaka huu sambamba na kuongeza ushirikiano kwa minajili ya kuhitimisha mkwamo wa sasa wa kisiasa wa nchi hiyo.
-
Juhudi za kuandaa sheria na kufanyika uchaguzi nchini Libya
Jan 11, 2023 02:32Kufanyika uchaguzi nchini Libya na kuingia madarakani serikali yenye ridhaa ya wananchi na kwa mujibu wa mchakato wa demokrasia ndio takwa kuu na la kimsingi la wananchi wa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Libya yawahukumu kifo wanachama 17 wa ISIS
Dec 20, 2022 07:12Mahakama moja nchini Libya imewahukumu kifo wanachama 17 wa kundi la kigaidi la ISIS (Daesh).
-
Waziri Mkuu wa Libya akiri kuhusika katika kuhamishwa mshukiwa wa Lockerbie
Dec 17, 2022 03:14Waziri Mkuu wa Libya, Abdulhamid al-Dbaiba amekiri kuwa serikali yake imehusika katika kumhamishia wiki iliyopita nchini Marekani Abu Agila Mohammad Masud Kheir al-Marimi mshukiwa katika kesi ya mlipuko wa Lockerbie.
-
Libya: Hatutaruhusu kufunguliwa tena kwa kesi ya Lockerbie
Dec 16, 2022 08:04Waziri Mkuu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya ametangaza kuwa nchi hiyo haitaruhusu kesi ya Lockerbie kufunguliwa tena.
-
Don DeBar: Marekani ingali inadhibiti matukio ya Libya
Dec 12, 2022 10:42Mwandishi wa habari na mchambuzi mmoja wa masuala ya kisiasa wa Marekani amesema kufufuliwa kwa faili la shambulio la bomu la Lockerbie la mwaka 1986 kunaonesha wazi kuwa Washington ingali inadhibiti na kuingilia masuala ya ndani ya Libya.
-
Baraza Kuu la Libya lakosoa hatua za Waziri Mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa ya nchi hiyo
Nov 15, 2022 11:28Mkuu wa Baraza Kuu la Serikali ya Libya amesema kuwa, Waziri Mkuu wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya nchi hiyo anakwamisha mchakato wa kufanyika vikao vya baraza hilo.
-
Maiti 230 zagunduliwa katika makaburi ya umati Libya
Nov 10, 2022 11:15Mamlaka za Libya zimetangaza habari ya kugunduliwa miili 230 ya watu wasiojulikana katika makaburi ya umati katika mji wa Tarhuna, ulioko kusini mwa mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Haftar atishia kuanzisha vita vya kuikomboa Libya
Nov 02, 2022 02:46Kamanda wa linalojiita jeshi la taifa la Libya ametishia kuwa, iwapo juhudi za sasa za kupata suluhisho la amani la mgogoro wa Libya zitafeli, ataanzisha vita vikubwa vya kuikomboa nchi hiyo.
-
Umoja wa Mataifa wasisitiza dhamira yake ya kusitisha vita nchini Libya
Oct 28, 2022 02:53Mwakilishi Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya kwa mara nyingine amesisitiza dhamira ya taasisi hiyo ya kimataifa ya kusitisha vita nchini humo.