-
Afrika Kusini yaishambulia US kwa kutoa 'tahadhari ya shambulio la kigaidi'
Oct 29, 2022 07:26Viongozi wa Afrika Kusini wameikosoa serikali ya Marekani kwa kutoa tahadhari ya uwezekano wa kutokea shambulizi la kigaidi katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika.
-
DNA yamuokoa Mmarekani mweusi aliyefungwa 'kimakosa' miaka 38
Oct 29, 2022 07:19Raia mmoja wa Marekani mwenye asili ya Afrika ameachiwa huru baada ya kufungwa jela kwa karibu miongo minne kwa kosa ambalo hakulifanya.
-
Russia yaonya baada ya US kupeleka silaha mpya za nyuklia Ulaya
Oct 29, 2022 07:11Russia imekosoa vikali hatua ya Marekani ya kupeleka silaha mpya za kisasa za nyuklia za B61 katika kambi za Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) barani Ulaya na kuonya kuwa, ikilazimu, Moscow itatoa jibu kali kwa kitendo hicho.
-
Mashtaka rasmi ya Russia kwa Umoja wa Mataifa kuhusu maabara za silaha za kibiolojia za Marekani nchini Ukraine
Oct 28, 2022 22:54Russia imepeleka malalamiko yake rasmi kwa Umoja wa Mataifa kuhusu kuwepo kwa maabara za silaha za kibiolojia za Marekani nchini Ukraine. Vasily Nebenzia, mwakilishi wa kudumu wa Russia katika Umoja wa Mataifa, amethibitisha kwamba nchi yake imekusanya ushahidi wa kutosha kuhusu uwepo wa maabara ya silaha hizo za kibiolojia za Marekani huko Ukraine.
-
Russia: Kuwepo kikosi cha jeshi la Marekani nchini Romania ni tishio kubwa
Oct 27, 2022 09:48Ikulu ya Rais wa Russia, Kremlin, imetangaza kuwa kupelekwa kwa wanajeshi wa Marekani nchini Romania, karibu na mpaka wa Ukraine, ni tishio kwa Russia. Hatua hiyo imechukuliwa na Marekani zaidi ya miezi minane baada ya Moscow kuanza mashambulizi ya kijeshi nchini Ukraine.
-
Iran: Uungaji mkono wa Magharibi kwa Israel ni mfano mkubwa zaidi wa ukiukaji wa haki za binadamu
Oct 26, 2022 03:41Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amelaani shambulio la utawala ghasibu wa Israel katika mji wa Nablus katika Ukingo wa Magharibi huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kuutaja uungaji mkono usio na kikomo wa Marekani na nchi nyingine za Magharibi kwa utawala dhalimu wa Israel kuwa ni kielelezo kikubwa zaidi cha ukiukwaji wa haki za binadamu.
-
Iran: Vikwazo kwa wazalishaji gesi kuwa na matokeo hasi
Oct 25, 2022 23:02Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametahadharisha kuwa, hatua ya Wamagharibi ya kuziwekea vikwazo nchi zinazozalisha na kuuza nje ya nchi gesi itakuwa na matokeo hasi yasiyoweza kurekebishika.
-
Hizbullah: Saudia na Marekani zinakwamisha uchaguzi wa Rais wa Lebanon
Oct 25, 2022 07:29Afisa mwandamizi wa Harakati ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema balozi za Saudi Arabia na Marekani jijini Beirut zimekula njama na kuweka vizingiti vya kila aina ili kukwamisha uchaguzi wa rais, huku ikiwa imesalia wiki moja tu kabla ya kumalizika muhula wa Rais Michel Aoun wa nchi hiyo.
-
Maandamano ya kupinga siasa za Marekani nchini Ethiopia
Oct 25, 2022 06:27Sambamba na kushtadi mapigano nchini Ethiopia na kuvunjwa makubalianao ya usitishaji vita ya miezi mitano na kuwaka tena moto wa vita katika nchi hiyo, maelfu ya Waethiopia walifanya maandamano ya nchi nzima siku ya Jumamosi kulaani uingiliaji wa madola ya kigeni, hasa Marekani, katika masuala ya ndani ya nchi yao.
-
Hujuma za magaidi zaongezeka kwa 300% Afrika licha ya operesheni za US
Oct 24, 2022 00:32Ripoti mpya ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Pentagon) inaonesha kuwa, mashambulizi ya magenge ya wanamgambo yameongezeka kwa asilimia 300 katika nchi za Afrika katika kipindi cha muongo mmoja uliopita.