-
Sheikh Naim Qassim: Iran iliwasaidia wananchi wa Lebanon, lakini Marekani inawaadhibu
Sep 24, 2022 23:13Naibu Katibu Mku wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, Iran ilikuwa pamoja na wananchi wa Lebanon katika matatizo na masaibu na iliwasaidia, lakini Marekani inawaadhibu.
-
Upinzani wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa kundi la Marafiki wa Kutetea Hati ya Umoja wa Mataifa dhidi ya vikwazo vya upande mmoja
Sep 24, 2022 22:42Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Kundi la Marafiki wa Kutetea Hati ya Umoja wa Mataifa wamedhihirisha upinzani wao dhidi ya vikwazo vya upande mmoja, na kusisitiza juu ya kuheshimiwa mamlaka, ardhi na kujitawala kwa nchi huru. Mawaziri hao wamesisitiza hilo katika mkutano wao uliofanyika kando ya kikao cha 77 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mnamo Septemba 22 huko New York.
-
Iran yajibu matamshi ya kifidhuli ya waziri wa mambo ya nje wa Marekani
Sep 24, 2022 03:43Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametumia mtandao wa kijamii wa Twitter kujibu matamshi ya kifidhuli ya waziri wa mambo ya nje wa Marekani aliyejipa uthubutu wa kukosoa kile alichodai ni haki za binadamu nchini Iran.
-
Hotuba ya Biden katika Umoja wa Mataifa na lawama zisizo na msingi kuhusu masuala mbalimbali
Sep 23, 2022 03:33Katika hotuba yake kwenye Baraza Kuu la 77 la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatano, Rais Joe Biden wa Marekani aliashiria masuala mbalimbali na kufafanua msimamo wa Washington kuhusu masuala hayo.
-
Ebrahim Raisi: Wapalestina ndio wenye haki ya kuishi katika ardhi za Palestina
Sep 19, 2022 02:56Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, wananchi wa Palestina ndio wenye haki ya kujiamulia wenyewe mustakbali wao na ndio wenye haki ya kuishi katika ardhi hizo.
-
Kutochapishwa ripoti ya mateso ya CIA kwa kisingizio cha tishio kwa usalama wa taifa wa Marekani
Sep 18, 2022 21:55Ripoti ya Seneti ya Marekani kuhusu mpango wa kikatili wa utesaji na kuwahoji washukiwa wa ugaidi wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) chini ya anwani "Programu ya Kuhoji Iliyoboreshwa" haitachapishwa kwa sasa.
-
Aghalabu ya Wademocrat wanatilia shaka iwapo Biden atagombea urais 2024
Sep 18, 2022 03:40Akthari ya wafuasi na wanachama wa chama cha Democrat nchini Marekani wametilia shaka uwezekano wa Rais Joe Biden wa nchi hiyo wa kugombea muhula wa pili katika uchaguzi ujao wa rais wa mwaka 2024.
-
Rais Putin: Kampuni kubwa 80 za Russia kwenda Iran wiki ijayo
Sep 15, 2022 23:37Rais Vladmir Putin wa Russia amesema Moscow imefanya kila iwezalo kuhakikisha kuwa Iran inakua mwanachama kamili wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO).
-
Marekani yapiga ngoma ya vita kwa kuipa Taiwan 'msaada' wa kijeshi
Sep 15, 2022 23:32Bunge la Seneti la Marekani limepasisha muswada wa sheria inayotaka Taiwan kupewa msaada wa kijeshi wa mabilioni ya dola, hatua inayotazamiwa kuighadhabisha China.
-
Utafiti: Akthari ya Wamarekani wanasema Biden ameligawa taifa
Sep 15, 2022 23:31Aghalabu ya wapigakura nchini Marekani wanaamini kuwa, Rais Joe Biden wa nchi hiyo amewagawa Wamarekani katika utawala wake, badala ya kuwaunganisha.