-
Biden kuajiri wahudumu wa afya laki moja kufuatilia watu wenye maambukizi ya corona
Nov 28, 2020 01:07Vyombo vya habari vya Marekani vimeripoti kuwa, Joe Biden ana mpango katika serikali yake ijayo nchini humo kuajiri wahudumu wa afya wapya laki moja kwa lengo la kuwafuatilia wale wote wenye maambukizi ya virusi vya corona.
-
Kukosolewa madola ya Magharibi kwa kufanya njama za kuzusha machafuko Russia na Belarus
Nov 27, 2020 23:55Sergey Lavrov, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia ameyatuhumu madola ya Magharibi mwamba, yanaingilia masuala ya ndani ya Russia na Belarus na kuyalaumu pia kwa kutekeleza vikwazo vya upande mmoja na kuwachochea wananchi wa mataifa hayo ili waanzishe vurugu na machafuko.
-
Watu wa Trump wawatishia kifo wafanyakazi wa kampuni iliyohusika na uchaguzi Marekani
Nov 27, 2020 03:19Wafanyakazi wa shirika moja lililohusika na uendeshaji wa uchaguzi nchini Marekani kwa muda sasa wamekuwa wakinyanyaswa na kutishiwa kifo, tangu rais wa nchi hiyo, Donald Trump alipoanza kudai kuweko uchakakachuaji wa kura na udanganyifu mkubwa katika uchaguzi wa Novemba 3, 2020 nchini humo.
-
Foreign Policy: Iran ni imara zaidi ya walivyofikiria Marekani na Israel
Nov 26, 2020 23:14Gazeti moja la Marekani limetangaza kuwa, White House na utawala wa Kizayuni wa Israel walikosea katika mahesabu yao kuhusiana na Iran kwani Tehran ni imara zaidi ya walivyodhani viongozi wa Marekani katika siasa zao za kuliweketa taifa la Iran vikwazo vya kiwango cha juu kupindukia.
-
Serikali ya Trump yazidi kutoa vitisho kuhusu uwezekano wa Marekani kurejea katika JCPOA
Nov 26, 2020 22:59Mshauri wa Usalama wa Taifa wa serikali ya Donald Trump huko White House ameendelea kutoa vitisho alivyodai ni vya hatari ya Marekani kurejea katika mapatano ya kimataifa ya JCPOA.
-
Bashar al Jaafari akosoa wanajeshi wa Marekani kuendelea kupora maliasili za Syria
Nov 26, 2020 04:36Mwakilishi wa Syria katika Umoja wa Mataifa amekosoa wanajeshi vamizi wa Marekani kuendelea kupora maliasili za Syria yakiwemo mafuta na gesi.
-
Kuondoka askari wa Marekani nchini Iraq; msimamo wa serikali ya Baghdad na makundi ya mapambano
Nov 24, 2020 23:12Katika hali ambayo viongozi wa serikali ya Baghdad wanasema kuwa askari 500 wa Marekani wataanza kutoka katika ardhi ya Iraq miezi miwili ijayo, Sheikh Qais al-Khaz'ali, Katibu Mkuu wa Harakati ya Asaib Ahlul Haq, karibuni hivi alitetea silaha za harakati hiyo ya mapambano ya Kiislamu akisisitiza kuwa muhula wa usitishaji vita na Marekani umekwisha.
-
Hospitali elfu moja za Marekani zimejaa wagonjwa, haziwezi tena kutoa huduma
Nov 23, 2020 22:53Mkurugenzi wa Kitivo cha Usalama wa Afya cha Chuo Kikuu cha Johns Hopkins ametangaza kuwa, sasa hivi hospitali elfu moja zimeshajaa wagonjwa wa COVID-19 nchini humo na hazina tena uwezo wa kupokea wagonjwa zaidi.
-
Trump atakiwa kukubali matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi Joe Biden
Nov 23, 2020 04:40Mshirika wa karibu wa rais Donald Trump, ambaye pia aliwahi kuwa Gavana wa jimbo la New Jersey Chris Christie, amemtaka Trump kukubali matokeo ya uchaguzi uliompa ushindi mpinzani wake wa karibu Joe Biden.
-
Wamarekani wapatao milioni 100 wanakabiliwa na hatari ya kukumbwa na baa la njaa
Nov 22, 2020 08:58Ripoti za taasisi za serikali ya Marekani zinaonyesha kuwa maambukizi ya virusi vya corona yamewafanya raia wapatao milioni 100 wa nchi hiyo wakabiliwe na hatari ya kukumbwa na baa la njaa.