-
Harakati ya Muqawama ya Iraq yatahadharisha kuhusu kuchelewa Marekani kuondoka nchini humo
Oct 11, 2020 23:39Msemaji wa Harakati ya Kataeb Hizbullah ya Iraq ameashiria ombi la Marekani la kusitishwa operesheni zinazolenga vikosi vya nchi hiyo na kusisitiza kuwa: Wanamapambano wa Iraq hawatakaa kimya hata kidogo mkabala na kuchelewa Washington kuondoa wanajeshi wake katika ardhi ya Iraq.
-
Iran: Marekani ni kidhabi kwa kudai vikwazo vipya havilengi sekta ya afya
Oct 11, 2020 08:41Waziri wa Afya wa Iran amelaani hatua ya Marekani ya kuliwekea vikwazo shadidi taifa hili na kubainisha kuwa, utawala wa Washington umekubuhu kwa kusema uwongo, kwa madai yake kuwa vikwazo vipya dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu havilengi sekta ya afya na tiba.
-
Marekani yaiba tena mafuta ya Syria na kuyapeleka Iraq
Oct 11, 2020 08:36Msafara wa malori 20 ya Marekani yaliyobeba mafuta ghafi yaliyoibwa kutoka visima vya mafuta vya Syria umeelekea nchini Iraq.
-
Makundi jamii ya ulinzi yaundwa US kukabiliana na machafuko ya baada ya uchaguzi, silaha zanunuliwa kwa wingi
Oct 10, 2020 04:26Baadhi ya raia wa Marekani ambao wanahofia uwezekano wa kutokea machafuko baada ya uchaguzi wa rais wameamua kuunda makundi jamii ya ulinzi, huku wengine wakikimbilia kwenye maduka ya silaha ili kununua bunduki kwa ajili ya usalama wao.
-
Vikwazo vipya vya Marekani, njama za juu zaidi za serikali ya Trump dhidi ya wananchi wa Iran
Oct 09, 2020 23:03Baada ya Marekani kujitoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA mwezi Mei 2018, White House imewawekea wananchi wa Iran vikwazo vya kiwango cha juu na hadi hivi sasa bado viongozi wa Washington wanaendelea kuongeza vikwazo hivyo.
-
Pelosi ataka faili la hali ya kiafya ya Trump liwekwe wazi, Trump asema ni kichaa
Oct 09, 2020 23:02Spika wa Kongresi ya Marekani Nancy Pelosi amesema kuwa Wamarekani wana haja ya kujua hali ya kiafya ya Rais Donald Trump akiashiria maradhi yake ya virusi vya corona na kulazwa hospitalini kwa siku kadhaa.
-
Ahadi mpya za Trump za kuondoa wanajeshi Afghanistan; ahadi chapwa za kiuchaguzi
Oct 09, 2020 07:05Uchaguzi wa Rais nchini Marekani unazidi kukaribia huku hali ya kisiasa ya rais wa nchi hiyo, Donald Trump si nzuri mbele ya mpinzani wake Joe Biden. Ikulu ya White House na hasa Trump mwenyewe wanazidi kufanya lolote liwezekanalo, hata kutoa ahadi za maneno tena zenye migongano, ili kuvutia wapiga kura.
-
Zarif: Njama za Marekani za kuwaua Wairani kwa njaa ni jinai dhidi ya binadamu
Oct 09, 2020 04:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekosoa vikali hatua ya Marekani ya kuiwekea Jamhuri ya Kiislamu vikwazo vipya vya kibenki na kusisitiza kuwa, taifa hili bila shaka litavuka salama udhalimu na ukatili huu mpya wa Washington.
-
Ravanchi: Mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa ya Marekani ni sawa na ugaidi wa kiserikali
Oct 09, 2020 04:14Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa ameyataja mashinikizo ya kiwango cha juu kabisa ya Marekani kuwa ni sawa na ugaidi wa kiserikali na kueleza kuwa: Sera hizo zimeratibiwa lengo likiwa ni kuwasababishia mashaka na masaibu wananchi na pia kusababisha machafuko ya kijamii kwa mujibu wa siasa hizo za kifisadi ili kubadili serikali.
-
Borell akiri udharura wa Iran kunufaika na mkataba wa JCPOA
Oct 09, 2020 03:43Licha ya kuwa Umoja wa Ulaya na Troika ya Ulaya ambayo inajumuisha nchi za Ujerumani, Ufaransa na Uingereza zilikuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha mapatano ya nyuklia ya Iran yanayojulikana kama JCPOA, lakini baada ya Marekani kujitoa katika mapatano hayo, pande hizo zimekuwa na utendaji mbaya usioweza kutetewa kutokana na kuwa zimeshindwa kuyalinda na pia kutotekeleza ahadi zao, na hasa kuhusu kutofanikisha mfumo wa mabadilishano ya kifedha na kibiashara unaojulikana kama Instex.