-
Kukiri John Bolton juu ya kugonga mwamba siasa za Marekani dhidi ya Venezuela
May 19, 2020 05:54Vikwazo na mashinikizo ya Marekani dhidi ya Venezuela yanaendelea katika hali ambayo, kivitendo nchi hiyo ya Amerika ya Latini ikipata msaada wa mataifa kama Iran, China na Russia imefanikiwa kuyapatia ufumbuzi akthari ya matatizo yaliyosababishwa na vikwazo vya Washington.
-
Sisitizo la Russia juu ya kutoweza Marekani kurejesha vikwazo vya kimataifa dhidi ya Iran
May 19, 2020 02:52Tarehe 8 Mei 2018, Marekani ilijitoa kijeuri katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia yanayojulikana kwa jina maarufu la JCPOA, lakini hivi sasa inafanya njama kubwa za kujaribu kuzuia utekelezaji wa makubaliano hayo hasa kipengee cha kuondolewa Iran vikwazo vya silaha kwa mujibu wa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hapo tarehe 18 Oktoba mwaka huu wa 2020. Hata hivyo wajumbe wa Mashariki wa kundi la 4+1 yaani Russia na China wamepinga vikali njama hizo za Marekani.
-
Mahathir bin Mohamad: Marekani inauza duniani ndege zake za kivita zenye ubovu
May 18, 2020 21:56Waziri Mkuu wa zamani wa Malaysia amefichua kwamba serikali ya Marekani iliiuzia nchi hiyo ndege za kivita za F16 huku zikiwa hazina namba maalumu wala vifaa muhimu na kwamba Washington huwa inatekeleza siasa hizo kwa nchi zote za dunia isipokuwa utawala haramu wa Kizayuni.
-
Onyo la Pompeo kwa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC katika kuunga mkono utawala wa Israel
May 18, 2020 04:55Tokea aingie madarakani huko White House, Rais Doland Trump amekuwa akichukua hatua zenye utata mkubwa katika kuunga mkono bila masharti yoyote, utawala ghasibu wa Israel kwa madhara ya taifa madhlumu la Palestina, jambo ambalo marais wengine wa zamani wa Marekani walijiepusha kulitekeleza hadharani.
-
Indhari ya António Guterres juu ya taathira hasi ya tofauti za China na Marekani kwenye juhudi za kukabiliana na Corona
May 17, 2020 20:02Kuenea kwa virusi vya Corona duniani bado kumewafanya watu kuwa wahanga, huku hofu yake ikibainisha kwamba janga hilo litazizidishia matatizo ya kiuchumi na kijamii nchi nyingi za dunia.
-
Onyo la Steven Mnuchin juu ya uwezekano wa kusambaratika uchumi wa Marekani
May 17, 2020 07:51Kuenea kwa virusi vya Corona nchini Marekani kumeisababishia jamii ya nchi hiyo matatizo makubwa ya kila upande hususan kwenye upande wa uchumi.
-
Pentagon ina wasiwasi Marekani itashindwa endapo itaingia vitani na China
May 17, 2020 03:31Baadhi ya duru katika Wizara ya Ulinzi ya Marekani Pentagon zimeonya kuwa kutokana na mazoezi ya karibuni kabisa yaliyofanywa na jeshi la nchi hiyo, endapo jeshi hilo litaingia vitani na China katika Bahari ya Mediterania litashindwa katika vita hivyo.
-
Theluthi mbili ya wanaoamini Mungu Marekani: Corona ni ujumbe unaotoka kwa Mungu
May 17, 2020 03:30Matokeo ya uchunguzi mpya wa maoni uliofanywa nchini Marekani yanaonyesha kuwa, baada ya kuzuka mripuko wa maradhi ya Covid-19, zaidi ya asilimia 65 ya raia wa nchi hiyo wanaoamini Mungu wamefikia hitimisho kuwa Mwenyezi Mungu anawahutubu kwamba wabadilike katika maisha yao.
-
Ombi la Umoja wa Mataifa kuhusu kuondolewa vikwazo dhidi ya Iran
May 17, 2020 02:17Baada ya serikali ya Rais Donald Trump kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) mwaka 2018 katika fremu ya sera za mashinikizo ya juu kabisa na kisha kushadidisha vikwazo ambavyo havijawahi kushuhudiwa katika historia dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na licha ya kuibuka ugonjwa wa COVID-19 nchini Iran, lakini bado Trump anasisitiza kuendeleza vikwazo vyake vilivyo dhidi ya ubinadamu dhidi ya taifa hili.
-
Marekani yaiwekea Huawei vikwazo vipya, uhusiano na China wazidi kuharibika
May 16, 2020 03:09Serikali ya Marekani imeliwekea vikwazo vipya shirika kubwa la kiteknolojia la China Huawei na hivyo kupelekea uhusiano wake na China ambao umezorota kuwa mbaya zaidi.