-
Kukosolewa njama za Marekani za kukatiwa bajeti Shirika la UNRWA
Jan 17, 2020 23:23Tangu Rais Donald Trump wa Marekani ashike hatamu za uongozi na kuingia katika ikulu ya nchi hiyo White House, alichukua mkondo wa kuuunga mkono kibubusa na bila masharti yoyote utawala haramu wa Israel na siasa za kuwa dhidi ya Wapalestina.
-
Askari wa US waliojeruhiwa na makombora ya Iran wanatibiwa Ujerumani na Kuwait
Jan 17, 2020 03:54Licha ya utawala wa Washington hapo awali kudai kuwa hakuna askari wa Marekani aliyeuawa au kujeruhiwa katika majibu makali yaliyotolewa na Iran dhidi ya kambi mbili za kijeshi za nchi hiyo huko Iraq, lakini hivi sasa imefichuka kuwa, wanajeshi kadhaa wa US waliojeruhiwa walipekwa kwa usafiri wa ndege katika nchi za Ujerumani na Kuwait kwa ajili ya matibabu.
-
Meja Jenerali Baqeri: Marekani itapata jibu kali zaidi la Iran ikiendeleza mienendo yake hasi
Jan 17, 2020 00:00Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema iwapo Marekani itaendeleza chokochoko na mienendo yake hasi dhidi ya taifa hili, basi iwe tayari kupokea jibu kali zaidi la Iran ya Kiislamu.
-
Kufichuka siri ya Trump alivyoishinikiza Troika ya Ulaya itekeleze 'Utaratibu wa Kifyatuo' katika JCPOA
Jan 16, 2020 23:18Licha ya madai zinayotoa nchi za Ulaya kuhusu ulazima wa kulindwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, Troika ya nchi hizo inayoundwa na Ujerumani, Ufaransa na Uingereza, siku ya Jumanne ya tarehe 14 Januari iliamua kutekeleza utaratibu wa kusuluhisha mzozano katika JCPOA, ambao kimsingi unatoa kitisho kwa Iran cha kuwekewa tena vikwazo vya nyuklia vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Sisitizo la Maduro kuhusu uungaji mkono wa Marekani kwa magaidi na makundi yenye kuchupa mipaka ndani ya Venezuela
Jan 16, 2020 08:41Katika kipindi cha uongozi wa Rais Doland Trump, Marekani imehusika na njama nyingi za kuiondoa madarakani serikali ya mrengo wa kushoto ya Venezuela na Rais wake Nicolás Maduro ili kumweka madarakani kibaraka wa Washington na kiongozi wa upinzani nchini humo Juan Guaidó; na inatumia kila wenzo kwa ajili ya kufikia lengo hilo.
-
Zarif: Ulaya wameamua "kuitosa" JCPOA kwa kuhofia ushuru mpya wa Trump
Jan 16, 2020 07:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameandika ujumbe mkali katika mtandao wa kijamii wa Twitter kulaani udhaifu wa nchi za Ulaya mbele ya Marekani na kuandika: Nchi tatu za Ulaya zilizobakia kwenye mapatano ya nyuklia ya JCPOA zimeamua kuyatupa makubaliano hayo kwa kuhofia ushuru mpya ambao Trump ametishia kuziwekea ushuru mpya nchi za Ulaya.
-
IRGC: Iran imefanikiwa kudhibiti uwezo na nguvu za Marekani
Jan 15, 2020 23:01Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria wimbi la hivi karibuni la ushindi wa Iran dhidi ya Marekani na kusema kuwa, "Jamhuri ya Kiislamu imefanikiwa kuidhalilisha na kuzidhibiti nguvu za Marekani."
-
Russia: Mauaji ya Jenerali Soleimani yanakiuka mipaka yote ya sheria na utu
Jan 14, 2020 23:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kitendo cha Marekani cha kumuua kigaidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, aliyekuwa Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) kinakiuka misingi na mipaka yote ya ubinadamu na sheria.
-
Bwabwaja mpya za Trump kuhusiana na mauaji ya Luteni Jenerali Qassim Soleimani
Jan 14, 2020 23:18Januari 3 mwezi huu, Marekani ilichukua hatua ya kijinai na isiyo ya kisheria ya kumuua Luteni Jenerali Qassim Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) na Naibu Mkuu wa Harakati ya Wananchi ya Hashd al-Shaabi ya Iraq pamoja na watu waliokuwa wamefuatana nao.
-
Misimamo ya kugongana ya Washington kuhusu sababu za kumuua kigaidi Luteni Soleimani
Jan 14, 2020 00:58Tarehe 3 Januari 2020, Marekani ilifanya jinai na ugaidi mkubwa wa kumuua kidhulma Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu tena akiwa mgeni rasmi wa serikali ya Iraq.