-
Vitisho vya Trump vya kuiwekea vikwazo Iraq, kushindwa kwingine kwa Washington
Jan 07, 2020 04:14Jinai kubwa ya Marekani ya kumuua kigaidi Meja Jenerali Qassem Soleimani na Abu Mahdi Al-Muhandis, Naibu Mkuu wa Harakati ya Kujitolea ya Wananchi wa Iraq ya Hashdu sh-Sha'abi nchini Iraq, imeibua radiamali kali ya bunge la nchi hiyo ya Kiarabu na kuipelekea kupitisha sheria ya kuvitimua vikosi vya muungano vamizi wa eti kupambana na Daesh (ISIS) unaojumuisha askari wa Marekani.
-
Vitisho vipya vya Trump kutokana na wahka wa ulipizaji kisasi wa Iran
Jan 05, 2020 23:13Hatua ya kijinai na iliyo kinyume cha sheria ya Marekani ya kumuua shahidi Jenerali Qassem Soleimani na Abu Mahdi al Muhandis Naibu Mkuu wa Harakati ya Hashdu sh-Sha'abi ya Iraq pamoja na shakhsia wengine huko mjini Baghdad, imekabiliwa na radiamali kali kutoka kwa Iran ambayo imesisitizia kulipiza kisasi kikali kwa Marekani.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran; Ulimwengu mzima una wajibu wa kukabiliana na hatua ya kigaidi ya Marekani
Jan 05, 2020 23:10Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema kuwa ulimwengu mzima una wajibu wa kukabiliana na hatua ya kigaidi ya Marekani ya kumuua shahidi Kamanda Qassem Soleimani; na watu wote wanapaswa kutekeleza majukumu yao mbele ya jinai hiyo.
-
Nasrullah: Siku ya kuuawa shahidi Kamanda Soleimani, mwanzo wa historia mpya Mashariki ya Kati + Video
Jan 05, 2020 12:26Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, tarehe 3 Januari 2020 ambayo ni siku ya kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH, ni mwanzo wa historia mpya katika eneo la Mashariki ya Kati.
-
Ukosoaji wa Russia dhidi ya njama za Marekani za kubadili mlingano wa nguvu Asia Magharibi na kuongeza vitisho vya usalama kimataifa
Jan 05, 2020 09:51Hatua za Marekani katika eneo la Asia Magharibi hususan za kuzidisha uwepo wake kijeshi, mashinikizo dhidi ya Iran na hatimaye kutekeleza hatua za kigaidi hasa za kumuua shahidi Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la IRGC, Naibu Mkuu wa Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Shaabi, Abu Mahdi al Muhandes na shakhsia wengine walioambatana nao, zimekabiliwa na radiamali kali kutoka kwa Russia kama mmoja wa wacheza karata muhimu katika eneo hili.
-
Wamarekani waandamana kulaani uchu wa vita wa utawala wa Trump
Jan 05, 2020 04:27Maelfu ya wanaharakati na wananchi wa Marekani wamefanya maandamano katika makumi ya miji ukiwemo mji mkuu Washington, kulaani hatua ya utawala wa Donald Trump ya kumuua shahidi kamanda wa jeshi la Iran, Luteni Jenerali Soleimani, pamoja na hatua ya Washington ya kutuma maelfu ya askari katika eneo la Asia Magharibi.
-
Malaysia: Marekani imetangaza vita kwa kumuua shahidi Soleimani
Jan 05, 2020 04:08Baraza la Shura la Jumuiya ya Waislamu Malaysia limelaani vikali hatua ya kigaidi ya Marekani ya kumuua shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC.
-
Kutapatapa viongozi wa Marekani ili kuhalalisha jinai yao ya kumuua shahidi kamanda Soleimani
Jan 04, 2020 08:13Viongozi wa ngazi ya juu wa Marekani wamedhihirisha misimamo ya kukinzana katika juhudi za kuhalalisha jinai yao ya kumuua kigaidi Kamanda Qassem Soleimani baada ya kudai kuwa eti hawataki vita na Iran.
-
Wairaqi walaani vikali kuuawa Qassem Soleimani na Abu Mahdi
Jan 03, 2020 23:20Shakhasia mbali mbali wa kisiasa na kidini nchini Iraq wamelaani vikali hujuma ya kigaidi ya Mareknai ambayo imepelekea Meja Jenerali Qassem Suleimani na Naibu Mkuu wa Harakati ya Kujitolea ya Wananchi wa Iraq (Al Hashd al Shaabi) Abu Mahdi la Muhandis kuuawa shahidi.
-
Bei za mafuta na dhahabu zapanda duniani kufuatia mauaji ya Jenerali Soleimani
Jan 03, 2020 08:45Bei za mafuta na dhahabu katika soko la kimataifa kote duniani zimepanda kufuatia kuuliwa shahidi Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran, Meja Jenerali Qassem Soleimani.