-
Licha ya kuafiki kusitisha mashambulio, ndege za kivita za Uturuki zaendelea kuua raia Syria
Oct 18, 2019 11:51Mashambulio ya anga yaliyofanywa na ndege za kivita za Uturuki yameua raia wasiopungua watano huku mapigano ya hapa na pale yakiendelea kati ya majeshi ya nchi hiyo na wapiganaji wa Kikurdi kaskazini mashariki mwa Syria licha ya maafikiano ya kusitisha hujuma yaliyofikiwa kati ya Uturuki na Marekani hapo jana.
-
Safari ya maafisa wa Marekani nchini Uturuki na kusalimu amri Ankara mbele ya matakwa ya Washington
Oct 18, 2019 10:55Mashambulizi ya jeshi la Uturuki huko kaskazini mwa Syria ambayo yamefanyika kwa ruhusa na baraka za Rais Donald Trump wa Marekani kwa kuyaondoa majeshi ya nchi hiyo katika eneo hilo, yamekabiliwa na upinzani mkali huko Washington kiasi kwamba, hata wawakilishi wa Kongresi wamepasisha azimio wakilaani hatua hiyo ya Trump.
-
Bunge la Marekani lalaani hatua ya Trump kuondoa wanajeshi wa Marekani Syria
Oct 17, 2019 23:53Hatua ya rais wa Marekani, Donald Trump ya kuondoa wanajeshi wa Marekani kaskazini mwa Syria, jambo ambalo limewezesha Uturuki kushambulia eneo hilo, imekosolewa ndani ya Marekani.
-
Iran: Kuzinduliwa ndege mpya ya kivita ya Yasin, ishara ya kushindwa vikwazo
Oct 17, 2019 10:03Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema hatua ya Iran kuzindua ndege mpya ya kivita iliyotengenezwa na wataalamu wa kijeshi wa hapa nchini ni ishara tosha kuwa vikwazo vya kidhalimu vya Marekani havijakuwa na athari zozote kwa taifa hili.
-
Rais Tayyip Erdoğan: Uturuki haiogopi vikwazo vya Marekani
Oct 17, 2019 09:52Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki amedai kwamba lengo la operesheni za nchi yake kaskazini mwa Syria lipo wazi na kwamba serikali ya Ankara haiogopi hata kidogo vikwazo vya Marekani.
-
Hali mbaya kwa wanajeshi wa Marekani Syria, Washington yalazimika kushambulia kambi zake yenyewe
Oct 17, 2019 04:33Baada ya wanajeshi vamizi wa Marekani kulazimika kuondoka kaskazini mwa Syria, jeshi hilo vamizi limeamua kushambulia na kuteketeza kila kitu katika kambi zake ambazo linalazimika kuondoka kaskazini mwa Syria.
-
China yaitahadharisha Marekani kwa kuingilia masuala ya ndani ya Hong Kong
Oct 16, 2019 08:32Serikali ya China imeendelea kulaani vikali uingiliaji wa Marekani katika masuala ya ndani ya mji wa Hong Kong, kwa kupasisha muswada uliopewa jina la 'Haki za binaadamu na demokrasia.'
-
Korea Kaskazini: Hatutosalimu amri mbele ya Marekani
Oct 16, 2019 08:21Kiongozi wa Korea Kaskazini amekemea uhasama wa vikwazo na mashinikizo ya Marekani dhidi ya nchi yake na kusisitiza kwamba, kamwe serikali ya Pyongyang haitosalimu amri mbele ya Washington.
-
Athari za vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran zafika katika fukwe za Ulaya
Oct 16, 2019 01:04Vikwazo vya kidhalimu vya Marekani dhidi ya Iran vimeanza kuziathiri nchi za Ulaya kwa njia isiyo ya moja kwa moja.
-
Trump na uvamizi wa Uturuki kaskazini mwa Syria; kutoka kubariki hadi vikwazo
Oct 15, 2019 23:26Licha ya kwamba awali rais wa Marekani alibariki uvamizi wa kijeshi wa Uturuki huko kaskazini mwa Syria lakini hivi sasa amegeuka kikamilifu na kutoa amri ya kuwekewa vikwazo Ankara.