-
Utafiti: Akthari ya Wamarekani wanasema nchi inaelekea pabaya
Feb 02, 2019 21:57Utafiti mpya wa maoni unaonesha kuwa aghalabu ya wananchi wa Marekani wanahisi kuwa nchi yao iko katika mkondo mbaya, huku wengi wao wakikata tamaa.
-
Hashdu sh-Sha'abi yawapiga marufuku askari wa Marekani kufanya doria Mosul, Iraq
Feb 02, 2019 04:42Naibu Kamanda wa Operesheni wa Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi katika mkoa wa nchini Iraq Nineveh (Nainawa), kaskazini mwa Iraq amesema kuwa, askari wa harakati hiyo wamewazuia askari wa Marekani kufanya doria mjini Mosul, ambao ni makao makuu ya mkoa huo.
-
Kukwama mazungumzo ya kibiashara baina ya Marekani na China
Feb 02, 2019 03:52Rais wa Marekani, Donald Trump ameendeleza siasa zake za kujikumbizia kila kitu upande wake kwa madai ya kulinda uchumi wa Marekani na kwa mara nyingine ametishia kuziwekea ushuru mpya bidhaa za China zinazoingia nchini humo licha ya kwamba Beijing ni mshirika mkubwa wa kibiashara wa Washington.
-
Zarif: Mapatano yoyote na Marekani hayana thamani ya hata ya wino juu ya karatasi
Feb 01, 2019 23:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, uamuzi wa Marekani wa kujitoa kwa muda katika Mkataba wa Silaha za Nyuklia za Masafa ya Kati (INF) kati yake na Russia unafikisha ujumbe kwamba mkataba wowote ule na serikali ya Marekani hata uliopasishwa na Congress, hauna thamani ya hata ya wino juu ya karatasi.
-
Marekani yajiondoa rasmi 'kwa muda' katika mkataba wa INF
Feb 01, 2019 10:45Serikali ya Marekani imetangaza rasmi kusimamisha kwa muda utekelezaji wa mkataba wa Silaha za Nyuklia za Masafa ya Kati (INF).
-
Marekani yashindwa kuzuia uteuzi wa Bachelet kuwa Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa UN
Jan 31, 2019 22:51Jarida la Marekani la Foreign Policy limefichua kwamba, kabla ya kuteuliwa Michelle Bachelet kuwa Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Marekani ilifanya jitihada kubwa za kuzuia uteuzi huo lakini jitihada hizo zimeambulia patupu.
-
Onyo la Russia kuhusu kuingilia kijeshi Marekani mgogoro wa Venezuela
Jan 30, 2019 09:24Matukio ya kisiasa yaliyojiri karibuni katika nchi yenye utajiri mkubwa wa mafuta ya Venezuela na makabiliano yanayozidi kupamba moto baina ya wapinzani na serikali ya mrengo wa kushoto ya nchi hiyo yameingia kwenye awamu nyeti na hasasi.
-
Ripoti: Kiwango cha ufisadi kimekithiri Marekani katika utawala wa Trump
Jan 29, 2019 21:41Ripoti ya shirika la kutathmini viwango vya ufisadi duniani la Transparency International imesema kiwango cha ufisadi na visa vya rushwa vimeogezeka pakubwa nchini Marekani tangu Rais Donald Trump aingie madarakani.
-
Kuongezeka harakati za kisiasa za Russia Asia Magharibi; kukabiliana na hatua za Marekani
Jan 27, 2019 04:38Katika miaka ya karibuni Russia imezidisha pakubwa harakati zake katika eneo la Asia Magharibi na kaskazini mwa Afrika. Nukta muhimu kuhusu jitihada hizo za Russia ni kuimarisha uwepo wake wa kijeshi huko Syria tangu Septemba mwaka 2015 kwa lengo la kupambana na makundi ya kigaidi na kuiunga mkono serikali halali ya Syria.
-
Hizbullah ya Lebanon: Daima Uingiliaji wa Marekani umekuwa na madhara kwa mataifa mengine
Jan 26, 2019 23:06Mkuu wa mrengo wa kisiasa wenye mafungamano na Harakati ya muqawama katika bunge la Lebanon umelaani uingiliaji wa Marekani katika masuala ya ndani ya Venezuela na kusema kuwa, uingiliaji wa Washington daima umekuwa na madhara kwa mataifa mengine na ni doa ambalo linapaswa kusafishwa katika historia ya mwanadamu.