-
Baqaei: Marekani ijitayarishe kwa athari za hatua yoyote dhidi ya Iran
Mar 31, 2025 08:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametangaza katika ujumbe wake kwamba, tishio lolote la rais wa nchi la kuishambulia Iran kwa mabomu ni ukiukaji wa wazi na kiini cha amani na usalama wa kimataifa.
-
Marekani, Mshirika Asiyeaminika
Mar 30, 2025 23:09Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney, ambaye amemrithi Justin Trudeau, amesisitiza kwamba atajibu hatua za Marekani dhidi ya nchi hiyo katika nyanja za kiuchumi na kibiashara, na amekiri kwamba: "Marekani si mshirika wa kuaminika tena."
-
Araqchi: Mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Yemen yanadhihirisha namna nchi hiyo inavyoshiriki katika uvunjaji wa sheria wa Israel
Mar 30, 2025 03:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amelaani mashambulizi ya kijeshi ya mara kwa mara ya Marekani katika maeneo mbalimbali ya Yemen na kusema: Mashambulizi ya kijeshi ya Marekani huko Yemen sambamba na kushtadi mauaji ya kimbari ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza na hujuma zake dhidi ya Lebanon na Syria, yanaonyesha namna Marekani inavyoshiriki katika uvunjaji sheria wa Israel na kwenda sambamba na utawala huo katika kueneza machafuko na hali ya mchafukoge katika eneo.
-
Wanachuo 300 wapokonywa viza US kwa kuiunga mkono Palestina
Mar 30, 2025 02:59Marekani imebatilisha viza za wanafunzi zaidi ya 300 wa kigeni kwa kuratibu na kushiriki katika maandamano ya kuwanga mkono na kuwatetea wananchi madhulumu wa Palestina katika mabewa ya vyuo vikuu kote nchini humo.
-
Zelenskyy: Ukraine imepokea pendekezo jipya la Marekani kuhusu makubaliano ya madini
Mar 29, 2025 23:07Rais wa Ukraine amesema kuwa Kiev imepokea pendekezo jipya kutoka Marekani kuhusu makubaliano ya madini.
-
Taasisi ya Wanafikra ya Marekani: Trump hawezi kuishinda Ansarulllah ya Yemen
Mar 29, 2025 07:16Taasisi ya Kutetea Demokrasia (FDD) nyenye makao yake makuu huko Washington DC imezungumzia kushindwa serikali ya Donald Trump katika kukabiliana barabara na harakati ya Ansarullah ya Yemen na kusisitiza kuwa: Serikali ya Trump inakabiliwa na hitilafu kubwa za ndani kuhusu Yemen, na muhimu zaidi, kuhusiana na Iran; na jambo hii ni moja ya sababu inayoikwamisha Marekani kuibuka na ushindi huko Yemen.
-
Marekani na Ulaya zashindwa kukabiliana na changamoto za kimataifa
Mar 28, 2025 02:34Mark Rutte, Katibu Mkuu wa NATO amesisitiza juu ya umoja wa pande mbili za Bahari ya Atlantiki na kusema kuwa changamoto za kiusalama duniani ni kubwa kiasi kwamba Ulaya na Marekani pake yazo haziwezi kukabiliana nazo.
-
Kukiri jamii ya ujasusi ya Marekani kwamba Hamas haijashindwa huko Gaza
Mar 27, 2025 22:57Ripoti kuhusu vitisho ambayo hutolewa kila mwaka na jamii ya masuala ya ujasusi ya Marekani imekiri kwamba kundi la muqawama wa Palestina la Hamas huko Gaza halijashindwa bado na kwamba linaendelea kudumisha nguvu, wapiganaji na miundombinu yake.
-
Cuba: Uhamiaji umekuwa biashara kwa Marekani
Mar 27, 2025 22:56Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba amepinga viza ya kadi ya dhahabu ya kupewa makazi mkabawa wa dola milioni tano ya Marekani, na kuituhumu serikali ya Trump kwa kutumia suala la uhamiaji kama biashara, kwa kuuza nyumba na kuwafukuza wahamiaji haramu.
-
Kutozwa ushuru wa asilimia 25 na Marekani kwa nchi zinazonunua mafuta ya Venezuela
Mar 27, 2025 02:19Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza kutoza ushuru wa asilimia 25 kwa biashara yoyote na nchi zinazonunua mafuta na gesi ya Venezuela. Ameelezea ushuru huu kama jibu la kutumwa Marekani wanachama wa genge la uhalifu la "Tren de Aragua".