-
Iraq yatoa onyo baada ya US kufanya mashambulizi ya anga nchini humo
Feb 03, 2024 03:58Serikali ya Iraq imelaani vikali mashambulizi ya anga yaliyofanywa na ndege za kivita za Marekani dhidi ya maeneo kadhaa ya nchi hiyo na nchi jirani yake Syria na kusisitiza kuwa, hujuma hizo zimekiuka mamlaka ya kujitawala ya nchi hiyo.
-
Ansarullah: US kuiasa China iingilie kadhia ya Bahari Nyekundu ni ishara ya kufeli
Feb 02, 2024 04:19Kiongozi wa Harakati ya Muqawama ya Ansarullah ya Yemen amesema juhudi za Washington za kutafuta usaidizi na upatanishi wa China ili iwaombe Wayemen wasimamishe mashambulizi dhidi ya meli za Marekani na Uingereza zinazopita Bahari Nyekundu zinaonesha namna madola hayo mawili ya kibeberu yalivyofeli katika mipango yao.
-
Iran yaitaka Marekani iache kutumia lugha ya vitisho dhidi yake
Feb 01, 2024 07:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameitaka Marekani iache kutumia lugha ya vitisho dhidi ya taifa hili na kusisitiza kuwa, vitisho vyovyote dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu vitakabiliwa na jibu madhubuti na la haraka.
-
Vikosi vya Yemen vyashambulia tena manowari ya US kwa makombora
Feb 01, 2024 07:36Msemaji wa Jeshi la Yemen amesema vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo vimefanya shambulio jipya la makombora dhidi ya meli ya kivita ya Marekani katika pwani ya Bahari Nyekundu.
-
Gazeti la US: Wanajeshi wa US walioko Iraq wamewekwa tayari kwenda kuisaidia Israel katika vita vya Gaza
Jan 31, 2024 09:42Gazeti la mtandaoni la The Intercept limeripoti kuwa, wanajeshi wa Marekani walioko nchini Iraq wamewekwa tayari ili itakapohitajika wakatoe msukumo na msaada katika mashambulio ya vita vya nchi kavu vya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza uliozingirwa.
-
Ukraine ina wasiwasi wa kupunguziwa misaada ya Magharibi
Jan 31, 2024 07:21Rais wa Ukraine amekiri kuwa jeshi la nchi hiyo ni dhaifu mkabala wa Russia na kusema: Ulaya peke yake haiwezi kuisaidia Ukraine dhidi ya Russia bila uungaji mkono wa Marekani.
-
Kushitakiwa Biden katika mahakama ya California kwa kuunga mkono mauaji ya kimbari
Jan 29, 2024 03:34Sambamba na kuendelea jinai za Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Ghaza na sambamba na hatua ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ ya kutoa hukumu dhidi ya utawala wa Kizayuni kwa jinai zake hizo, hivi sasa wimbi la kulaani jinai za Wazayuni na waungaji mkono wake nalo linazidi kuwa kubwa, siku baada ya siku.
-
Askari 3 wa Marekani wauawa, 30 wajeruhiwa Jordan; Muqawama wa Iraq wathibitisha kuhusika
Jan 29, 2024 00:19Askari watatu wa jeshi la Marekani wameuawa katika shambulio la ndege zisizo na rubani kwenye kambi ndogo ya jeshi hilo iliyoko nchini Jordan.
-
Trump: Iwapo Marekani itashambuliwa, NATO haitakuja kuiokoa
Jan 28, 2024 23:32Rais wa zamani wa Marekani amesema kwamba, haitakidi kuwa Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi NATO litaenda kuikoa Marekani iwapo nchi hiyo itakabiliwa na mashambulizi.
-
Biden ashtakiwa Marekani kwa "kushiriki" mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel Gaza
Jan 28, 2024 02:48Mahakama moja ya mji wa Oakland katika jimbo la California, imesikiliza mashtaka yaliyofunguliwa dhidi ya Rais wa Marekani Joe Biden na maafisa kadhaa waandamizi wa nchi hiyo ya "kushiriki katika mauaji ya kimbari yanayofanywa na Israel Gaza".