-
Iran kujiunga na mfumo wa BRICS PAY ili kukwepa vikwazo vya Marekani
Oct 01, 2023 03:52Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Qalibaf amesema Iran itajiunga na BRICS PAY, mfumo wa kibenki wa kielektroniki unaotumiwa na muungano wa BRICS wa mataifa yanayoinukia kiuchumi, ili kukwepa vizuizi vya kibenki vilivyosababishwa na vikwazo vya Marekani.
-
Bashar Assad: Marekani inashirikiana na magaidi
Sep 30, 2023 03:46Rais Bashar al-Assad wa Syria amezungumzia kuwepo kwa magaidi katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa nchi hiyo na jinsi Marekani ilivyo na udhibiti kamili wa maeneo hayo na kusisitiza kwamba Washington inashirikiana na magaidi.
-
Waziri wa Russia: BRICS itaanzisha mfumo mbadala wa SWIFT
Sep 30, 2023 01:08Waziri wa Fedha wa Russia amedokeza kuwa, nchi wanachama wa kundi la BRICS zinajiandaa kuanzisha mfumo wa mawasiliano ya kibenki kama mbadala wa ule wa SWIFT wa Wamagharibi.
-
Onyo la Guterres kuhusu ushindani na hatari ya vita vya nyuklia duniani
Sep 28, 2023 04:23Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameonya kuhusu dunia kuingia katika mashindano mapya ya silaha za nyuklia ambayo yanaweza kueneza maafa duniani kote. Katika siku ya mwisho ya mkutano wa mwaka wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Katibu Mkuu wa Baraza la Usalama amesema mashindano ya silaha yanatia wasiwasi wa kuongezeka karibuni idadi ya silaha za nyuklia ulimwenguni.
-
Kukiri kwa Borrell kwamba nchi zinazoendelea zinatafuta mbadala wa Magharibi
Sep 26, 2023 04:00Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya, Josep Borrell, ameandika katika makala iliyochapishwa kwenye blogu yake akisema: "Sheria zinazotawala dunia zinachakaa na nchi zinazoendelea za kusini mwa dunia zinatafuta mbadala wa Magharibi."
-
Hatua mpya ya Russia ya kutumia sarafu za kitaifa na kupunguza utegemezi kwa dola ya Marekani
Sep 22, 2023 22:48Serikali ya Russia imeidhinisha orodha ya nchi 31, zikiwemo Iran, Brazil, Venezuela na Cuba, ambazo benki zao zinaweza kushiriki na kufanya biashara katika soko la fedha za kigeni nchini Russia.
-
Raisi: Mradi wa kuufanya ulimwengu uwe wa Kimarekani umefeli
Sep 19, 2023 23:51Rais Ebrahim Raisi wa Iran amesema mpango wa Marekani wa kuitwisha dunia sera na misimamo yake umefeli na kugonga mwamba.
-
Mabadilishano ya wafungwa na kuendelea misimamo ya Marekani dhidi ya Iran
Sep 19, 2023 23:07Kufuatia mafanikio ya kubadilishana wafungwa kati ya Iran na Marekani Jumatatu ya juzi, raia watano wa Iran ambao walifunguliwa mashtaka kinyume cha sheria na vyombo vya mahakama vya Marekani kutokana na shughuli za kawaida za kibiashara waliachiliwa huru.
-
"Marekani haiwezi kustahamili sauti ya vyombo huru vya habari"
Sep 19, 2023 22:51Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (IRIB) ametoa radiamali yake kwa hatua ya karibuni ya Marekani ya kuviwekea vikwazo vyombo vitatu vya habari vya Iran ikiwemo kanali ya Press TV na kusisitiza kuwa, "Marekani kamwe haiwezi kuvumulia sauti ya vyombo huru vya habari."
-
Waislamu Marekani waishtaki FBI kwa orodha ya 'siri' ya kutotumia ndege
Sep 19, 2023 10:08Kundi la kuwatetea Waislamu nchini Marekani limeishtaki Idara ya Upelelezi, FBI, katika jaribio la kukomesha utumiaji wa orodha ya siri ambayo aghalabu inalenga Waislamu pekee kwa uchunguzi wanaposafiri kwa ndege.