-
Kukata tamaa Marekani na Nato kuhusu ushindi wa Ukraine katika vita na Russia
Sep 18, 2023 23:00Jenerali Mark Milley, mkuu wa majeshi ya Marekani, amesema ni vigumu kufikia natija ya haraka kuhusu vita vya Ukraine na kwamba muda mrefu zaidi unahitajika kabla ya Ukraine kufikia ushindi huo.
-
Njama za Marekani za kuongeza uwepo wake wa kijeshi nchini Yemen
Sep 18, 2023 08:49Tangu mazungumzo kati ya Yemen na Saudi Arabia kuhitimisha vita yalipochukua mkondo wa azma ya kweli, harakati za kijeshi za Marekani na Uingereza nazo zimeongezeka na kuimarika ili kuimarisha uwepo wao wa kijeshi katika nchi hiyo.
-
Rais wa Sierra Leone asema Marekani ilimshinikiza kuingilia uchaguzi wa nchi hiyo
Sep 17, 2023 04:40Rais Julius Maada Bio wa Sierra Leone aliituhumu Marekani Ijumaa kuwa ilimshinikiza kuingilia mchakato wa uchaguzi wa nchi hiyo uliofanyika June 24, kauli ambayo inapingana na msimamo ambao umekuwa ukionyeshwa na serikali ya Washington kuhusiana na kuwa huru uchaguzi wa nchi hiyo.
-
Iran: Tutajibu mapigo ya vikwazo vipya vya Umoja wa Ulaya
Sep 17, 2023 01:08Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo kwa hatua ya kujikariri ya Umoja wa Ulaya na Uingereza ya kuendelea kulisakama taifa hili kwa vikwazo.
-
Al-Shabaab ya Somalia yaitishia Marekani, yasema italipiza kisasi
Sep 17, 2023 01:07Kiongozi mwandamizi wa kundi la kigaidi la al-Shabaab la Somalia ameionya Marekani kufuatia shambulizi la anga la hivi karibuni lililofanywa na ndege za kivita za US kusini mwa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Uvunjaji ahadi mwingine wa Troika ya Ulaya kuhusu mapatano ya JCPOA
Sep 16, 2023 22:55Kupitia taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya Umoja wa Ulaya Alhamisi usiku, Josep Burrell, mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya alitangaza kuwa nchi tatu za Ulaya, ambazo ni Uingereza, Ufaransa na Ujerumani, zimemwandikia barua zikitangaza kwamba hazitaondoa vikwazo vya makombora dhidi ya Iran, ambavyo muda wake umepangwa kumalizika tarehe 18 Oktoba 2023.
-
Iran: Mauaji ya kinyama ya Sabra na Shatila ni doa la aibu kwa waungaji mkono wa utawala wa Kizayuni
Sep 16, 2023 08:46Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya mauaji ya Wapalestina wa Sabra na Shatila yaliyofanywa na askari wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ameandika ujumbe usemao: Sabra na Shatila daima litabaki kuwa doa la aibu kwenye vipaji vya waungaji mkono wa utawala wa Israel na watetezi wa kizandiki wa haki za binadamu hususan Marekani na Uingereza.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran asema wizi wa mafuta uliofanywa na serikali ya Marekani haukubaliki
Sep 16, 2023 04:39Waziri wa Ulinzi wa Iran amezungumzia hatua ya serikali ya Marekani ya kutwaa meli ya mafuta ya Iran na kupora bidha iliyokuwemo akisema: Hatua ya serikali ya Marekani ni wizi ambao haukubaliwi kwa namna yoyote ile duniani.
-
Mkuu wa majeshi ya Marekani akiri rasmi kuwa wameshindwa katika vita vya Afghanistan
Sep 15, 2023 22:55Mkuu wa majeshi ya Marekani Jenerali Mark Milley amekiri kuwa vita ilivyoanzisha nchi hiyo huko Afghanistan vimeishia kwa kushindwa vikosi vya jeshi hilo.
-
Hatua mpya ya Baraza la Wawakilishi la Marekani dhidi ya Iran; jaribio la kuzidisha mashinikizo
Sep 15, 2023 22:45Baraza la Wawakilishi la Marekani limepitisha mpango wa kiuadui dhidi ya Iran unaojulikana kama "Sheria ya Mahsa" kwa kura 410 za ndio na 3 za hapana. Mpango huo unailazimu serikali ya Marekani kuwawekea vikwazo maafisa wakuu wa Iran kwa kisingizio cha haki za binadamu, na wakati huo huo kupiga marufuku kuingizwa na kuuzwa nje silaha za Iran.