-
UN yashindwa tena kulaani jinai za Israel huko Gaza, yatosheka kwa kueleza masikitiko
May 16, 2021 02:13Sambamba na mashambulizi makali na ya kinyama yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya makazi ya raia wa Ukanda wa Gaza, na mauaji ya raia katika eneo hilo, Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine tena umeshindwa kuchukua hatua ya maana ya kusimamisha mashambulizi hayo au hata kulaani kwa maneno hujuma na ukatili huo wa Israel.
-
Makundi ya kutetea haki za binadamu yapinga uamuzi wa Ufarasa wa kupiga marufuku maandamano dhidi ya Israel
May 14, 2021 08:07Wanaharakati na makundi ya kutetea haki za binadamu yamepinga uamuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani wa Ufaransa wa kupiga marufuku maandamano ya kupinga ukatili na mauaji yanayofanywa na Israel dhidi ya watu wa Palestina ambayo yamepangwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii.
-
Arsenal yamtetea Elneny kwa kuwaunga mkono Wapalestina, yasema wachezaji wana haki ya kueleza maoni yao
May 14, 2021 05:30Klabu ya soka ya Arsenal nchini Uingereza imemtetea mchezaji wake Muislamu raia wa Misri, Mohamed Elneny aliyetuma ujumbe kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter akiwaunga mkono na kueleza mshikamano wake na watu wa Palestina wanaoendelea kushambuliwa na kuuawa na jeshi la utawala haramu wa Israel.
-
Waziri Mkuu wa Sudan alaani mauaji ya maandamano mjini Khartoum
May 13, 2021 02:37Waziri Mkuu wa Sudan Abdalla Hamdok amesema "ameshtushwa" na mauaji ya waandamanaji wanaotetea haki za Wasudani waliouawa na askari usalama miaka miwili iliyopita na ameyataja mauaji ya sasa kuwa ni "uhalifu wa kutumia risasi hai dhidi ya watu wanaoandamana kwa amani".
-
Kufichuliwa mambo mapya kuhusiana na Marekani kumuua kigaidi Luteni Jenerali Soleimani
May 10, 2021 05:00Jumamosi usiku, tovuti ya habari ya Yahoo News iliandika makala na ndani yake ilitoa taarifa mpya kuhusu operesheni ya jinai ya kinyama iliyofanywa na jeshi la kigaidi la Marekani ya kumuua shahidi aliyekuwa kamanda wa kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH, Luteni Jenerali Qassem Suleimani.
-
Jeshi la Chad lasema limeua 'mamia ya waasi'
May 01, 2021 08:23Baraza la kijeshi linalotawala Chad katika kipindi cha mpito limedai kuwa limeua mamia ya waasi katika makabiliano makali ya siku mbili huko mashariki mwa nchi, ambako aliyekuwa rais wa nchi hiyo Idriss Deby aliuawa.
-
AU, UN na EU zalaani mauaji ya Rais Idriss Deby wa Chad
Apr 21, 2021 03:10Umoja wa Afrika (AU), Umoja wa Mataifa (UN) na Umoja wa Ulaya (EU) zimelaani na kukosoa vikali mauaji ya Rais Idriss Deby Itno wa Chad.
-
Askari polisi aliyemuua Mmarekani mweusi, George Floyd apatikana na hatia
Apr 21, 2021 01:29Derek Chauvin, afisa mzungu wa polisi wa Marekani ambaye alimuua kikatili Mmarekani mwenye asili ya Afrika, George Floyd na kuzusha maandamano makubwa ya kupinga ubaguzi wa rangi dunia nzima hatimaye amepatikana na hatia katika mashitaka yote ya mauaji yaliyokuwa yakimuandama.
-
Rais Idriss Deby wa Chad auawa kabla ya kuapishwa kwa awamu ya sita
Apr 20, 2021 08:38Jeshi la Chad limetangaza leo kuwa rais wa nchi hiyo, Idriss Deby ameuawa kutokana na majeraha aliyoyapata katika medani ya vita.
-
Jumamosi, 10 Aprili, 2021
Apr 09, 2021 21:59Leo ni Jumamosi tarehe 27 Shaaban 1442 Hijria inayosadifiana na tarehe 10 Aprili 2021 Miladia.