-
IFJ: Waandishi habari karibu mia moja wameuawa mwaka 2018 duniani
Jan 01, 2019 23:20Shirikisho la Kimataifa la Waandishi wa Habari (IFJ) limetangaza kuwa, waandishi habari 94 waliuawa mwaka uliomalizika wa 2018 katika maeneo mbalimbali ya dunia.
-
Magaidi wa ADF waendeleza mauaji Kongo DR kuelekea uchaguzi
Dec 12, 2018 03:05Watu 10 wameripotiwa kuuawa katika mashambulizi yaliyofanywa na kundi la wanamgambo wa ADF mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
Khashoggi na waandishi habari wengine, Watu Mashuhuri mwaka huu
Dec 11, 2018 21:40Jarida la kila wiki la Marekani la Time limemteua mwandishi habari na mkosoaji wa utawala wa Saudi Arabia Jamal Khashoggi kuwa ndiye Mtu Mashuhuri wa Mwaka huu (Person of the Year) wa jarida hilo.
-
Wazayuni watoa wito wa kuuliwa kigaidi Mahmoud Abbas
Dec 11, 2018 12:13Watu wasiojulikana wameanza kusambaza matangazo na kutundika makaratasi katika vituo vya upekezi vinavyodhibitiwa na askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukingo wa Magharibi wakitaka kuuliwa Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Mahmoud Abbas.
-
Mshauri wa zamani: Saudia iliidhinisha mauaji ya Yassir Arafat
Dec 11, 2018 03:18Aliyekuwa mshauri mwandamizi wa Yasser Arafat, Rais wa zamani wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amefichua kuwa kiongozi huyo wa zamani wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina (PLO) hakufa kifo cha kawaida baada kuugua, bali aliuawa, na kwamba Saudi Arabia ndiyo iliyoidhinisha mauaji yake.
-
Seneta Graham: Kukana kwamba Bin Salman aliamuru kuuawa Khashoggi ni kujifanya kipofu
Dec 04, 2018 21:41Seneta mashuhuri wa Marekani Lindsey Graham amekosoa vikali siasa za Saudi Arabia na Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa nchi hiyo Muhammad bin Salman na kusisitiza kuwa, Kongresi ya Marekani itachukua msimamo mkali ili kukomesha sera mbovu za Riyadh bila ya kujali msimamo wa serikali ya Rais Donald Trump.
-
Kadhia ya mauaji ya Jamal Khashoggi yajadiliwa katika kikao cha haki za binaadamu mjini Paris
Oct 30, 2018 22:57Kadhia ya mauaji ya Jamal Khashoggi, mwandishi wa habari mkoasoaji wa utawala wa Saudi Arabia, imepewa uzingatiaji na kikao cha dunia cha haki za binaadamu mjini Paris, Ufaransa.
-
Mshauri wa Rais wa Uturuki apinga riwaya ya Saudia kuhusu mauaji ya Khashoggi
Oct 22, 2018 12:53Mshauri wa Rais wa Uturuki amepinga madai yaliyotolewa na Saudi Arabia kuhusu mauaji ya mwanadishi na mkosoaji wa utawala wa nchi hiyo Jamal Khashoggi huku nchi za Magharibi zikiendelea kutilia shaka taarifa ya Riyadh kuhusu mauaji hayo.
-
Hujuma za kigaidi zalipuka tena Msumbiji, 12 wauawa
Sep 21, 2018 09:16Kundi la kigaidi linaloaminika kuwa na mfungamano na al-Shabaab ya Somalia limevamia kijiji kimoja katika mkoa wa Cabo Delgado kaskazini mwa Msumbiji na kuua watu 12 na kujeruhiwa wengine kadhaa.
-
Kuuawa kiongozi wa upinzani wa eneo lenye mamlaka ya ndani la Donetsk, Ukraine na athari zake
Sep 02, 2018 05:53Kufuatia kuuawa Alexander Zakharchenko, Kiongozi wa Upinzani wa eneo la Donetsk nchini Ukrain, Rais Vladmir Putin wa Russia ametaka kuchukuliwa hatua kali wahusika wa jinai hiyo.